Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 10:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Upepo mukali unapopita na mwovu anatoweka, lakini mwenye haki anaimarishwa milele.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 10:25
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata hivyo, mutu wa haki anashika njia yake, mutu ambaye hajafanya ubaya kwa mukono wake anazidi kuwa na nguvu.


Atatoweka kama ndoto, asionekane tena, atafutikana kama maono ya usiku.


Hata hivyo, wapeperushwe kama majani yenye kukauka, wakuwe kama maganda yanayopelekwa na zoruba!


Wimbo wa safari za kidini. Wanaomutegemea Yawe, wako kama mulima Sayuni, ambao hautikisiki lakini unabaki imara siku zote.


Mbele hawajatambua, waongolewe kama miiba, michongoma au magugu. Kwa hasira ya Mungu, wapeperushwe mbali, wakikuwa bado wazima.


watoweke kama konokono anavyoyeyuka akitembea, kama mimba iliyoharibika isiyoona jua hata kidogo!


Wenye haki hawataondolewa katika inchi hata kidogo, lakini waovu hawatakaa katika inchi.


Mutu hawezi kudumu katika kutenda maovu, lakini hakuna kitu kinachoweza kumwangusha mutu wa haki.


Waovu wanaangamizwa na kutoweka kabisa, lakini jamaa ya wenye haki itasimama.


Mara tu wanaposimikwa na kuanza kuota, hata mbele hawajatoa mizizi kama miti katika udongo, Yawe akiwapulizia wananyauka, upepo mukali unawapeperusha kama makapi!


Nami sasa ninakuambia: ewe Petro, wewe ni jiwe, na juu ya jiwe hili, nitajenga musingi wa kanisa langu, na hata uwezo wa lufu hautaweza kulishinda.


Ninyi vilevile ni kama jengo linalosimama juu ya musingi uliowekwa na mitume na manabii; Yesu Kristo mwenyewe ndiye jiwe kubwa la pembe.


Kwa njia hii, watajiwekea akiba nzuri na yenye kudumu kwa ajili ya siku zitakazokuja kusudi wapate uzima wa kweli.


Lakini musingi uliojengwa na Mungu, unasimama imara. Nayo maneno haya yamechapwa juu ya musingi ule “Bwana anajua wale wanaokuwa wake,” na haya mengine: “Kila mutu anayesema kwamba yeye ni wa Bwana anapaswa kujitenga na maovu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ