Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 10:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Kitu mutu mwovu anachoogopa ndicho kitakachomupata, lakini kitu mwenye haki anachotamani ndicho atakachopewa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 10:24
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sauti za vitisho zitamupigia kelele katika masikio. Anapozani amestawi, mwangamizi atamushambulia.


Kile ninachoogopa kimenipata; ninachohofu ndicho kilitokea.


Anajibia mahitaji yao wote wanaomwabudu; anasikia kilio chao na kuwaokoa.


Ee Yawe, mufalme anashangilia kwa nguvu yako, anafurahi sana kwa musaada uliomupa.


Uitafute furaha yako kwa Yawe, naye atakujalia unayotamani katika moyo.


Kwa sababu hiyo, woga utakapowapata kama zoruba, hasara yenu itakapowatokea kama upepo mukali, taabu na huzuni vitakapowapata, nitachekelea hasara yenu na kuwasimanga.


Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maombi ya watu wa usawa yanamufurahisha Mungu.


Basi, nitawaletea taabu; zile hasara zote wanazoogopa zitawapata; maana nilipoita hakuna aliyeitika, niliposema hawakunisikiliza. Lakini walifanya maovu mbele yangu, walichagua yale ambayo hayanipendezi.


Ninyi mumeogopa upanga? Basi, mimi nitaleta upanga juu yenu! –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Alipokuwa angali anasema maneno hayo, sauti kutoka mbinguni ikamwambia: Ewe mufalme Nebukadneza, sikiliza ujumbe huu juu yako! Umenyanganywa ufalme!


Heri wale wanaokuwa na njaa na kiu ya kufanya yanayokuwa haki, maana watashibishwa!


“Sitawaacha kama wayatima, nitawarudilia tena.


Mpaka sasa hamujaomba kitu kwa jina langu. Muombe, nanyi mutapewa, na furaha yenu itakuwa kubwa kabisa.


Lakini inayobaki tu ni kungojea kwa woga hukumu na moto mukali wa Mungu utakaowateketeza waasi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ