Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 10:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Baraka za Yawe ndizo zinazoleta utajiri. Juhudi za mutu haziongezi kitu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 10:22
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, nitakubariki na kutukuza jina lako, nawe utakuwa baraka.


Wakati ule, Abramu alikuwa ametajirika sana. Alikuwa na makundi ya nyama, feza na zahabu.


kwamba sitatwaa uzi au kamba ya kiatu, wala chochote kinachokuwa chako, kusudi usijivune na kusema kwamba umenitajirisha.


Yawe amemubariki sana bwana wangu, naye amekuwa mutu mukubwa. Amemupa makundi ya kondoo na nyama wengi, feza na zahabu, watumishi wanaume na wanawake, ngamia na punda!


Mwaka ule Isaka akapanda mbegu katika inchi ile, akavuna mara mia zaidi, maana Yawe alimubariki,


naye akatajirika. Alizidi kupata mali mpaka akakuwa tajiri sana.


Umwambie, Yawe anasema hivi: ‘Umeua na kutwaa mali yake vilevile?’ Umwambie Yawe anasema hivi: ‘Pahali pale imbwa walipoilambulia damu ya Naboti, ndipo watakapoilambulia damu yako.’ ”


Lakini Yebesi alimwomba Mungu wa Israeli akisema: “Ee Mungu, ninakusihi unibariki na kupanua mipaka yangu. Mukono wako ukuwe pamoja nami na unilinde kutokana na jambo lolote ovu, na mateso yasinipate.” Naye Mungu akamupa yale aliyoomba.


Amazia akamwuliza yule mutu wa Mungu: “Tutafanya nini na feza yote ambayo nimekwisha wapa waaskari wa Israeli?” Naye akamujibu: “Yawe anaweza kukupa zaidi ya hiyo.”


Mufalme Hezekia akatajirika sana na kuheshimiwa. Alijitengenezea hazina za feza, za zahabu, za mawe ya bei kali za viungo, ngao na za aina zote za vyombo vya bei kubwa.


Vile vile alijiongezea miji kwa ajili yake mwenyewe, makundi mengi ya ngombe na kondoo kwa sababu Yawe alimupa mali nyingi.


Aliwabariki watu wake, wakaongezeka; na hesabu ya wanyama wao akaizidisha.


Munajisumbua bure kuamuka asubui mapema na kuchelewa kwenda kupumzika magaribi, mujipatie chakula kwa jasho lenu. Mungu anatimiza mahitaji ya wapendwa wake hata wanapolala.


Waliobarikiwa na Yawe watarizi inchi, lakini waliolaaniwa naye wataongolewa.


Mali ni taji ya utukufu wa wenye hekima, lakini ujinga ni kitambaa cha wapumbafu.


Mali iliyopatikana kwa haraka kwa mwanzo, haitakuwa ya heri kwa mwisho.


Mutu muchoyo anakimbilia mali, wala hajui kwamba ukosefu utamufikia.


Ninawatajirisha wale wanaonipenda, ninajaza tele hazina za wanaonipenda.


Kisha siku hizo kumi, aliwaangalia akaona kwamba wale vijana waliokula mboga za majani walionekana wenye afya na nguvu kuliko wale wengine wote waliokulishwa chakula cha kifalme.


Yawe wa majeshi anasema kwamba yeye mwenyewe ataipeleka laana hiyo. Itapenya kila nyumba ya mwizi na kila nyumba ya mwenye kuapa uongo kwa kutumia jina lake; itakaa mule na kuteketeza nyumba hiyo yote, mbao na mawe.


Na sasa ninamuletea Yawe malimbuko ya mazao ya inchi ambayo amenipa’. “Kisha utaweka kikapu chini, mbele ya Yawe, Mungu wako, na kuabudu mbele yake.


Yawe atawafanikisha kwa wingi: watoto, mifugo na mavuno katika shamba katika inchi aliyowaapia wazee wenu kwamba atawapa.


Lakini musitwae kitu chochote ambacho kimetolewa kusudi kiangamizwe. Mukitwaa kitu chochote ambacho kimetolewa kusudi kiangamizwe, mutaifanya kambi ya Israeli kuwa kitu cha kuangamizwa, na hivyo kuiletea hasara.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ