Yawe amemubariki sana bwana wangu, naye amekuwa mutu mukubwa. Amemupa makundi ya kondoo na nyama wengi, feza na zahabu, watumishi wanaume na wanawake, ngamia na punda!
Umwambie, Yawe anasema hivi: ‘Umeua na kutwaa mali yake vilevile?’ Umwambie Yawe anasema hivi: ‘Pahali pale imbwa walipoilambulia damu ya Naboti, ndipo watakapoilambulia damu yako.’ ”
Lakini Yebesi alimwomba Mungu wa Israeli akisema: “Ee Mungu, ninakusihi unibariki na kupanua mipaka yangu. Mukono wako ukuwe pamoja nami na unilinde kutokana na jambo lolote ovu, na mateso yasinipate.” Naye Mungu akamupa yale aliyoomba.
Amazia akamwuliza yule mutu wa Mungu: “Tutafanya nini na feza yote ambayo nimekwisha wapa waaskari wa Israeli?” Naye akamujibu: “Yawe anaweza kukupa zaidi ya hiyo.”
Mufalme Hezekia akatajirika sana na kuheshimiwa. Alijitengenezea hazina za feza, za zahabu, za mawe ya bei kali za viungo, ngao na za aina zote za vyombo vya bei kubwa.
Munajisumbua bure kuamuka asubui mapema na kuchelewa kwenda kupumzika magaribi, mujipatie chakula kwa jasho lenu. Mungu anatimiza mahitaji ya wapendwa wake hata wanapolala.
Kisha siku hizo kumi, aliwaangalia akaona kwamba wale vijana waliokula mboga za majani walionekana wenye afya na nguvu kuliko wale wengine wote waliokulishwa chakula cha kifalme.
Yawe wa majeshi anasema kwamba yeye mwenyewe ataipeleka laana hiyo. Itapenya kila nyumba ya mwizi na kila nyumba ya mwenye kuapa uongo kwa kutumia jina lake; itakaa mule na kuteketeza nyumba hiyo yote, mbao na mawe.
Lakini musitwae kitu chochote ambacho kimetolewa kusudi kiangamizwe. Mukitwaa kitu chochote ambacho kimetolewa kusudi kiangamizwe, mutaifanya kambi ya Israeli kuwa kitu cha kuangamizwa, na hivyo kuiletea hasara.