Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 1:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Mwenye hekima akizisikiliza, zitamwongezea elimu; na mwenye ufahamu zitamupatia ujuzi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 1:5
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Na alipokuwa angali akisema naye, Amazia akamwambia: “Nyamaza! Tulikufanya wewe kuwa mushauri wa mufalme? Kwa nini uawe?” Nabii akanyamaza, lakini akasema: “Ninafahamu kwamba Mungu ameamua kukuangamiza kwa maana umetenda haya yote, kisha unazarau shauri langu.”


Kwa hiyo munisikilize, enyi wenye ujuzi. Mungu hawezi kufanya uovu hata kidogo; Mungu Mwenye Uwezo hawezi kufanya kosa.


Kama una akili sikiliza; sikiliza ninachokuambia.


Musikilize maneno yangu, enyi wenye hekima, munitegee masikio yenu, ninyi wenye ujuzi.


Mutu yeyote mwenye akili, na kila mwenye hekima anayenisikiliza atasema:


Anayependa mafundisho anapenda maarifa, lakini asiyependa kuonywa ni mujinga.


Mwenye mazarau anatafuta hekima naye haipati, lakini mwenye akili anapata maarifa kwepesi.


Mutu mwenye akili anajipatia maarifa; sikio la mwenye hekima linatafuta maarifa.


Umwazibu mwenye kuzarau naye mujinga atapata akili; umwonye mwenye akili naye atapata maarifa.


Mwenye kiburi anapoazibiwa, mujinga anapata hekima. Ukimufundisha mwenye hekima, unamupatia maarifa.


Musikilize mafundisho mupate hekima, wala musiyakatae.


Usimwonye mwenye kiburi maana atakuchukia; umwonye mwenye hekima naye atakupenda.


Umufundishe mwenye hekima naye atazidi kuwa na hekima; umufundishe mutu wa haki naye atazidi kuwa na elimu.


Tena, nimeona kitu kimoja hapa chini ya jua, kwamba wenye kukimbia mbio hawashindi katika mashindano ya kukimbia, wala wenye nguvu hawashindi vita, wenye hekima hawapati chakula, wenye akili hawatajiriki, wala wenye ujuzi hawapandi vyeo. Lakini wakati wa bahati unawapata wote pamoja.


Ninasema nanyi kama watu wenye akili; muamue ninyi wenyewe juu ya maneno ninayotaka kuwaambia:


Mushike na kutimiza masharti na maagizo hayo maana mukifanya hivyo watu wa mataifa mengine watakapopata kujua masharti hayo, watatambua kwamba ninyi ni wenye hekima na akili. Watasema hivi: ‘Kweli watu wa taifa hili kubwa wana hekima na akili!’


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ