Ewe kijana, furahia ujana wako, moyo wako ukuwe na raha wakati ungali kijana. Fuata mapenzi ya moyo wako na tamaa ya macho yako. Lakini kumbuka kwamba Mungu atakuhukumu kadiri ya hayo yote.
Humo kutakuwa barabara kubwa, nayo itaitwa Njia Takatifu. Watu wachafu hawatapitia humo, lakini wale watu wa Mungu tu; wapumbafu hawatakanyaga ndani yake,
Mushike na kutimiza masharti na maagizo hayo maana mukifanya hivyo watu wa mataifa mengine watakapopata kujua masharti hayo, watatambua kwamba ninyi ni wenye hekima na akili. Watasema hivi: ‘Kweli watu wa taifa hili kubwa wana hekima na akili!’