Lakini wao waliendelea kuwachekelea wajumbe wa Mungu, wakayazarau maneno yake na kuwachekelea manabii wake mpaka kwa mwisho kasirani ya Yawe ikawaka juu ya watu wake hata hakukukuwa wa kuwaponyesha.
Nilipokuja, kwa nini sikukuta mutu? Nilipoita mbona hamukuitikia? Mukono wangu ni mufupi hata nisiweze kuwaokoa ninyi? Sina nguvu ya kuwakomboa? Ninakausha bahari kwa kuikaripia, na mito ninaifanya kuwa jangwa; samaki wake wanakufa na kunuka kwa kukosa maji.
Basi, nitawaletea taabu; zile hasara zote wanazoogopa zitawapata; maana nilipoita hakuna aliyeitika, niliposema hawakunisikiliza. Lakini walifanya maovu mbele yangu, walichagua yale ambayo hayanipendezi.
Kwa hiyo, Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi: Ninawaletea Wayuda na wakaaji wote wa Yerusalema hasara zote nilizosema juu yao, kwa sababu mimi nilisema nao, lakini hawakunisikiliza; niliwaita, lakini hawakuniitikia.
Kwa sababu ya mambo hayo watasikia uzito wa kasirani yangu. Sitamwacha hata mutu mumoja aponyoke wala sitamwonea huruma mutu yeyote. Hata wakinililia kwa sauti kubwa mimi sitawasikiliza.