Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mezali 1:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 “Enyi wajinga! Mpaka wakati gani mutapenda kuwa wajinga? Mpaka wakati gani wenye kuzarau watafurahia mazarau yao, na wapumbafu kuchukia maarifa?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mezali 1:22
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ni nani anayekuwa kama Yobu ambaye kwake mazarau ni kama kunywa maji?


Heri mutu asiyefuata shauri la waovu, asiyeshiriki katika njia ya wenye zambi, wala kukusanyika na wenye kuzarau;


Enyi wajinga wa mwisho, mufikiri kidogo! Enyi wapumbafu, mutapata akili wakati gani?


Basi, Musa na Haruni wakamwendea mufalme wa Misri na kumwambia: “Yawe, Mungu wa Waebrania, anasema hivi: ‘Mpaka wakati gani utakataa kujinyenyekeza mbele yangu? Uwaache watu wangu waondoke kusudi wanitumikie.


Hapo Yawe akamwambia Musa: “Mpaka wakati gani mutakataa kutii amri na sheria zangu?


inaita kwenye masanganjia, inaita kwenye milango ya muji:


“Muliyachukia maarifa, wala hamukuchagua kumwogopa Yawe,


Maana wajinga wanajiua kwa kiburi chao, wapumbafu wanajiangamiza kwa kufanikiwa kwao.


Zitawaerevusha wajinga, zitawapa vijana maarifa na akili.


Kumwogopa Yawe ni musingi wa maarifa, lakini wapumbafu wanazarau hekima na mafundisho.


Mwenye mazarau anatafuta hekima naye haipati, lakini mwenye akili anapata maarifa kwepesi.


Mwenye mazarau hapendi kuonywa, hatafuti hata kidogo maoni ya wenye hekima.


Azabu iko tayari kwa wenye kuzarau, na mapigo kwa migongo ya wapumbafu.


Mwenye kiburi anapoazibiwa, mujinga anapata hekima. Ukimufundisha mwenye hekima, unamupatia maarifa.


Mwenye kiburi na majivuno jina lake ni “Mazarau”; anatenda kwa kujivuna tu.


Mwenye akili anaona hatari na kujificha, lakini wajinga wanajitokeza mbele na kuumia.


Yeye anazarau wenye mazarau, lakini anakubali wanyenyekevu.


Kwa hiyo utasema: “Kwa nini nilichukia mafundisho? Kwa nini nilizarau ndani ya moyo wangu?


Ewe muvivu, utalala pale mpaka wakati gani? Utaamuka wakati gani katika usingizi wako?


nikawaona vijana wengi wajinga, na hasa mumoja aliyekuwa mupumbafu.


Enyi wajinga, mujifunze kuwa na akili; musikilize kwa uangalifu, enyi wapumbafu.


Nimeyaona machukizo yako: nimeona uzinzi wako na utongozaji wako, na uasherati wako usiousikilia haya, unaoufanya juu ya milima na katika mashamba. Ole kwako wewe Yerusalema! Mpaka wakati gani utabaki bila kutakaswa?


Wewe Yerusalema, usafishe maovu ya moyo wako, kusudi upate kuokolewa. Mpaka wakati gani utaendelea kuchunga maovu?


Kundi hili la watu waovu litaendelea kuninungunikia mpaka wakati gani? Nimechoka na haya manunguniko ya Waisraeli juu yangu!


Na Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ee ninyi watu wa kizazi kisichoamini Mungu na chenye kupotoka. Nitakaa pamoja nanyi tena mpaka wakati gani? Nitawavumilia tena mpaka wakati gani? Muniletee mutoto hapa.”


“Ewe Yerusalema, Ewe Yerusalema. Wewe unaua manabii na kuwatupia mawe wale ambao Mungu anakutumia. Mara nyingi nilitaka kuwakusanya wakaaji wako kama vile kuku anavyokusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake, lakini ninyi hamukutaka!


Muende kujifunza maana ya Maandiko Matakatifu yanayosema: ‘Ninataka huruma, lakini si sadaka zenu.’ Kwa maana sikukuja kuwaita wenye haki kunifuata, lakini watenda mabaya.”


akisema: “Kama wewe vilevile ungejua leo hii kitu kinachoweza kukuletea amani! Lakini sasa kitu hicho kimefichwa, nawe hauwezi kukiona!


Kila mutu anayefanya mabaya anachukia mwangaza, naye anakataa kuja kwenye mwangaza, kusudi matendo yake yasionekane wazi.


Mbele ya yote, mujue kwamba katika siku za mwisho kutakuja watu watakaoishi kufuatana na tamaa zao wenyewe. Watawachekelea ninyi


Roho na Bibi arusi wanasema: “Kuja!” Naye mwenye kusikia maneno haya aseme vilevile: “Kuja!” Yule anayesikia kiu akuje, na yule anayetaka maji ya uzima akuje kuyapokea kwa bure.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ