2 Zitawawezesha watu kujua hekima na mafundisho, na kufahamu misemo yenye maana kubwa.
Kumwogopa Yawe ni mafundisho ya hekima; mbele ya kuheshimika inafaa kuwa munyenyekevu.
Kupata hekima ni bora kuliko zahabu; kupata akili ni chaguo bora kuliko feza.
Kwa nini mupumbafu kuwa na feza katika mukono kwa kununua hekima, wakati yeye mwenyewe hana akili?
Sikiliza shauri na kupokea mafundisho, upate hekima ya kukufaa kwa siku zinazokuja.
Ukinisikiliza, utafahamu haki, usawa, na kufuata sheria ya Mungu; utafahamu kila njia nzuri.
Wana wangu, musikilize maadibisho ya baba yenu, mutege sikio mupate kuwa na akili.
Uambie Hekima: “Wewe ni dada yangu”, na Akili: “Wewe ni rafiki yangu”.
Musikilize mafundisho mupate hekima, wala musiyakatae.
Enyi wajinga, mujifunze kuwa na akili; musikilize kwa uangalifu, enyi wapumbafu.