kwa maana mimi ni pamoja nawe. Hakuna mutu katika muji huu atakayesubutu kukukamata kwa kukutendea vibaya, kwa maana ndani yake kutakuwa watu wengi watakaonigeukia.”
Naye Yesu anayeitwa Yusto, anawasalimia ninyi vilevile. Kati ya Wayuda walioamini ni hao watatu tu ndio wanaotumika pamoja nami kwa ajili ya kazi inayoelekea Ufalme wa Mungu, nao wamenifariji sana.
Wazee wa kanisa wanaoongoza kazi yao vizuri wanastahili kupokea mushahara mara mbili, hasa zaidi wale wanaojitolea kwa kufanya kazi ya kuhubiri na kufundisha.
Ninyi hamukulipa mishahara ya watumishi waliotumika katika mashamba yenu. Musikilize mashitaki yao! Malalamiko ya wavunaji yamefika katika masikio ya Bwana Mwenye Uwezo!