Lakini inatosha kwa mwanafunzi kufanana na mwalimu wake na mutumishi kufanana na bwana wake. Ikiwa wanamwita mukubwa wa jamaa Belzebuli, hawatakosa kuwaita watu wa jamaa yake kwa majina mabaya zaidi.
Ninyi munasema kwamba ninafukuza pepo kwa uwezo wa Belzebuli. Basi watu wa kikundi chenu wanawafukuza kwa uwezo wa nani? Watu hao wanashuhudia kwa njia ya matendo yao kwamba ninyi ni wakosaji!
Walimu wa Sheria waliotoka Yerusalema, wakasema hivi juu ya Yesu: “Amepatwa na Belzebuli.” Na wengine wao wakasema: “Ni huyo mukubwa wa pepo ndiye anayemupa uwezo wa kufukuza pepo.”