31 Lakini wakaenda na kuanza kutangaza habari za Yesu katika inchi ile yote.
Katika siku zile, Herode, liwali wa jimbo la Galilaya, akasikia habari za Yesu.
Basi wale waaskari walinzi wakapokea zile feza na kufanya sawa walivyoambiwa. Na habari hii ilienea katikati ya Wayuda mpaka leo.
Habari zake zikavuma katika inchi yote ya Suria. Wakamuletea watu wote walioteswa na magonjwa mbalimbali na wenye maumivu ya kila namna, wenye pepo, wenye kifafa na wenye kupooza, naye Yesu akawaponyesha.
Habari za jambo hili zikaenea katika inchi ile yote.
Halafu sifa za Yesu zikaenea upesi katika jimbo lote la Galilaya.
Yesu akawaagiza wasimwambie mutu habari ya tendo hili. Lakini kwa kadiri alivyowakataza, wao walizidi kutangaza habari.
Yesu akarudia Galilaya akijazwa na uwezo wa Roho, na habari zake zikaenea fasi zote katika pande zile.
Na habari za Yesu zikaenea katika jimbo lile lote.
Hata hivi habari juu ya Yesu zikazidi kuvuma na makundi mengi ya watu wakakusanyika kwa kumusikiliza na kuponyeshwa magonjwa yao.
Na jambo hili Yesu alilolifanya likaenea katika Yudea yote na katika inchi zote zinazokuwa pembeni.