29 Halafu Yesu akagusa macho yao, akisema: “Ifanyike kwenu sawa vile munavyoaminia.”
Halafu Yesu akamujibu: “Wewe mwanamuke, imani yako ni kubwa! Ifanyike kwako sawa ulivyoomba.” Na binti yake akapona tangia saa ile ile.
Yesu akawasikilia huruma. Akagusa macho yao, na mara moja wakapata kuona, nao wakamufuata.
Kisha Yesu akamwambia yule mukubwa wa waaskari hivi: “Urudie kwako, na ifanyike kwako sawa ulivyoamini.” Na saa ile ile mutumishi wake akapona.
Naye Yesu alipogeuka, akamwona na kumwambia: “Binti yangu, ujipe moyo! Imani yako imekuponyesha.” Na mwanamuke yule akapona saa ile ile.
Na wakati Yesu alipoingia ndani ya nyumba, wale vipofu wakamufikia. Naye akawauliza: “Munaamini kwamba ninaweza kuwafanyia jambo hilo?” Nao wakamujibu: “Ndiyo, Bwana.”
Yesu akamwambia: “Ujiendee, imani yako imekuponyesha.” Na pale pale akapata kuona, na kumufuata Yesu katika njia.