Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 9:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27 Yesu akaondoka toka pale, naye alipokuwa katika njia, vipofu wawili wakamufuata wakilalamika, wakisema: “Utuhurumie, Ee Mwana wa Daudi!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 9:27
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Haya ni majina ya babu za Yesu Kristo, wa uzao wa Daudi, wa uzao wa Abrahamu. Abrahamu alizaa Isaka, Isaka alizaa Yakobo, Yakobo alizaa Yuda na wandugu zake, Yuda alizaa Peresi na Zera kutoka muke wake Tamari, Peresi alizaa Hesironi, Hesironi alizaa Ramu, Ramu alizaa Aminadabu, Aminadabu alizaa Nasoni, Nasoni alizaa Salmoni, Salmoni alizaa Boazi kutoka muke wake Rahaba, Boazi alizaa Obedi kutoka muke wake Ruta, Obedi alizaa Yese, Yese alizaa mufalme Daudi, Daudi alizaa Solomono (mama yake ndiye yule aliyekuwa muke wa marehemu Uria), Solomono alizaa Rehoboamu, Rehoboamu alizaa Abiya, Abiya alizaa Asa, Asa alizaa Yosafati, Yosafati alizaa Yoramu, Yoramu alizaa Uzia, Uzia alizaa Yotamu, Yotamu alizaa Ahazi, Ahazi alizaa Hezekia, Hezekia alizaa Manase, Manase alizaa Amoni, Amoni alizaa Yosia, Yosia alizaa Yekonia na wandugu zake, wakati Waisraeli walipohamishwa kwenda Babeli. Nyuma ya kuhamishwa kwa Waisraeli kwenda Babeli, Yekonia alizaa Saltieli, Saltieli alizaa Zerubabeli, Zerubabeli alizaa Abihudi, Abihudi alizaa Eliakimu, Eliakimu alizaa Azoro, Azoro alizaa Zadoki, Zadoki alizaa Akimu, Akimu alizaa Elihudi, Elihudi alizaa Eleazari, Eleazari alizaa Matani, Matani alizaa Yakobo, Yakobo alizaa Yosefu, yule alikuwa mume wa Maria, mama ya Yesu, anayeitwa Kristo.


vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanapata kusikia, wafu wanafufuliwa na Habari Njema inahubiriwa kwa wamasikini.


Mwanamuke mumoja Mukanana aliyeishi katika pande zile akamufikia, akilalamika, akisema: “Ee Bwana, mwana wa Daudi, unihurumie! Binti yangu anateswa sana na pepo.”


na kusema: “Bwana, ninakuomba umusikilie mwana wangu huruma kwa maana anateswa sana na ugonjwa wa kifafa. Mara nyingi anaanguka katika moto na ndani ya maji.


Yesu na wanafunzi wake walipokuwa wakitoka Yeriko, kundi kubwa la watu wakamufuata.


Lakini wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria wakachukizwa kwa kuona miujiza aliyoifanya na watoto waliokuwa wakilalamika katika hekalu, wakisema: “Usifiwe wewe, mwana wa Daudi!”


Nalo kundi la watu waliomutangulia Yesu na lile la watu waliofuata nyuma yake, wakaanza kulalamika, wakisema: “Usifiwe wewe Mwana wa Daudi! Abarikiwe huyu anayekuja kwa jina la Bwana! Mungu asifiwe juu mbinguni!”


Na wakati Yesu alipoingia ndani ya nyumba, wale vipofu wakamufikia. Naye akawauliza: “Munaamini kwamba ninaweza kuwafanyia jambo hilo?” Nao wakamujibu: “Ndiyo, Bwana.”


Ubarikiwe ufalme unaokuja, ndio ufalme wa babu yetu Daudi! Mungu asifiwe juu mbinguni!”


Na mara nyingi huyu pepo anamutupa katika moto na ndani ya maji, kusudi amwue. Lakini kama unaweza kufanya kitu, utuhurumie na kutusaidia.”


wakilalamika, wakisema: “Yesu Bwana utusikilie huruma!”


Yesu akaongeza kuwaambia: “Namna gani wanaweza kusema kwamba Kristo ni Mwana wa Daudi?


Saa ile ile Yesu akawaponyesha watu wengi walioteswa na magonjwa na ulema mbalimbali pamoja na wenye pepo, na kuwaponyesha hata vipofu wengi.


Maandiko Matakatifu hayakusema kwamba Kristo atazaliwa katika ukoo wa mufalme Daudi na katika muji Betelehemu, pahali Daudi alipoishi?”


Habari hiyo inaelekea Mwana wake ndiye Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye alizaliwa kimwili katika uzao wa mufalme Daudi. Lakini kwa namna ya Roho Mutakatifu, alihakikishwa kwa uwezo kuwa yeye ni Mwana wa Mungu kwa njia ya kufufuka kwake.


Wao ni wazao wa babu zetu, na Kristo alizaliwa kimwili katika kizazi chao. Yeye ndiye mukubwa kupita wote na Mungu anayesifiwa kwa milele! Amina.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ