Nawe, muji Kapernaumu, unafikiri kwamba utapandishwa mpaka juu mbinguni? Utashushwa mpaka chini katika kuzimu. Kwa maana miujiza iliyofanyika ndani yako ingalifanyika katika Sodoma, muji ule ungekuwa ungali hata leo.
Mukubwa wa waaskari na wale waliokuwa pamoja naye wakimuchunga Yesu walipoona tetemeko la inchi na mambo yote yaliyofanyika, wakaogopa sana, na kusema: “Hakika mutu huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”
Lakini walipokwisha kumufunga Paulo na kamba kusudi wamupige, yeye akamwambia jemadari mumoja aliyekuwa pale: “Sheria inawaruhusu kumupiga mwanainchi wa Roma, ingawa hajahukumiwa bado?”
Kisha jemadari akawaita wakubwa wawili wa waaskari wake, akawaambia: “Mutayarishe waaskari mia mbili, waaskari wapanda-farasi makumi saba, na waaskari wapiga mikuki mia mbili kwa kwenda Kaisaria saa tatu ya usiku.
Upepo usiokuwa mukali ulipoanza kuvuma tokea kusini, wakazani kwamba wataweza tu kutimiza sawa walivyokuwa wamekusudia. Wakapandisha nanga na kuendelea pembenipembeni karibu sana na Krete.
Lakini kwa kuwa mukubwa wa jeshi alitaka kumuponyesha Paulo, yeye akawazuiza wasitimize kusudi lao. Akaamuru wale waliojua kuogelea wajitupe wa kwanza ndani ya maji na kuvuka mpaka inchi kavu.
Na kwa kuwa muji Luda ulikuwa karibu na muji Yopa, wanafunzi walikuwa wamesikia kwamba Petro yuko kule. Kwa hiyo wakatuma kwake wajumbe wawili kwa kumwambia: “Tunakusihi, ufike huku kwetu bila kukawia.”