Lakini Namani alikasirika sana, akaenda zake akisema: “Nilizani kwamba hakika atanifikia na kumwomba Yawe, Mungu wake, apitishe mikono yake juu ya pahali ninapogonjwa na kuniponyesha!
Basi, Namani akateremuka kwenye muto Yordani akajitumbukiza mule mara saba, kama alivyoagizwa na Elisha mutu wa Mungu, naye akapona kabisa. Ngozi yake ikakuwa laini na yenye afya kama ya mutoto mudogo.
Kisha Mungu akamwambia: “Ingiza tena mukono wako kwenye kifua chako!” Musa akaingiza mukono wake kwenye kifua. Alipoutoa inje, ukarudilia hali yake ya kawaida kama vile mwili wake unavyokuwa.
Wakati Yesu alipoona watu wengi wanazidi kukusanyika mbiombio, akamukaripia yule pepo na kumwambia: “Wewe pepo wa bubu na wa kiziwi, ninakuamuru utoke ndani ya mutu huyu wala usimurudilie tena!”
Vilevile kulikuwa watu wengi wenye ukoma katika Israeli katika siku za nabii Elisha, lakini hakuna mumoja kati yao aliyetakaswa, isipokuwa tu Namani wa inchi ya Suria.”
Kama nisingetenda kati yao matendo yasiyofanywa na mutu mwingine, wasingekuwa na zambi. Lakini sasa wameyaona lakini hata hivi wananichukia mimi pamoja na Baba yangu.