Matayo 8:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
29 Halafu wakaanza kulalamika wakisema: “Kuna maneno gani kati yako na sisi wewe Mwana wa Mungu? Umekuja hapa kwa kututesa mbele ya kutimia kwa wakati wetu?”
Lakini mufalme akamwambia: “Kuna maneno gani kati yangu na ninyi wana wa Zeruya? Ikiwa Yawe amemwambia: ‘Umulaani Daudi’, nani sasa anaweza kuuliza: ‘Kwa nini umefanya hivyo?’ ”
Yule mwanamuke akamwambia Elia: “Ewe mutu wa Mungu, kuna maneno gani kati yako nami? Kumbe ulikuja kwangu kwa kuzifichua zambi zangu na kusababisha kifo cha mwana wangu?”
Elisha akamwuliza mufalme wa Israeli: “Kuna maneno gani kati yako nami? Kwenda uombe shauri kwa manabii ambao baba yako na mama yako waliwaendea.” Mufalme wa Israeli akajibu: “Sivyo! Yawe ndiye aliyetuita sisi wafalme watatu kusudi atutie katika mikono ya mufalme wa Moabu.”
lakini mufalme Neko akamutumia ujumbe akisema: “Vita hivi havikuelekei wewe hata kidogo, ewe mufalme wa Yuda. Sikukuja kupigana nawe lakini na waadui zangu, na Mungu ameniamuru niharakishe. Acha basi kumupinga Mungu, ambaye yuko upande wangu, kama sivyo atakuangamiza.”
Pepo wakatoka ndani ya watu wengi, wakilalamika, wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakaripia, na hakuwaachilia waseme neno, kwa sababu walijua kwamba yeye ndiye Kristo.
Wakati alipomwona Yesu, akalalamika na kuanguka mbele yake, na kusema kwa nguvu: “Yesu, Mwana wa Mungu Mukubwa, kuna neno kati yako na mimi? Ninakusihi, usinitese!”
Mwanamuke yule akaendelea kumufuata Paulo na sisi, akilalamika akisema: “Watu hawa ni watumishi wa Mungu Mukubwa. Wanawatangazia ninyi namna gani munavyoweza kuokolewa.”
Kwa maana Mungu hakuwahurumia wale wamalaika waliofanya zambi, lakini aliwatupa katika jehenamu. Wao wanalindwa mule wakifungwa minyororo katika giza nzito wakingojea Siku ile ya hukumu.
Mukumbuke vilevile wamalaika wale waliokosa kulinda vema cheo chao, lakini wakaacha makao yao: Mungu akawaweka katika nafasi ya giza, wakifungwa minyororo ya milele kwa kungojea Siku ile ya hukumu.