24 Mara moja zoruba kubwa ikatokea katika ziwa na maji yakajitupatupa ndani ya chombo. Lakini Yesu alikuwa amelala usingizi.
Ewe Yerusalema, uliteseka, ulitaabishwa na kukosa wa kukufariji, lakini nitakujenga upya kwa mawe ya bei kali, misingi yako itakuwa ya mawe ya yakuti.
Milima ilikuona, ikanyauka; mafuriko ya maji yakapita mule. Vilindi vya bahari vilinguruma, na kurusha juu mawimbi yake.
Halafu Yesu akaingia ndani ya chombo, nao wanafunzi wake wakaenda naye.
Wanafunzi wake wakamujongelea, wakamwamusha na kumwambia: “Bwana, utuokoe! Tunakufa!”
Nao walipokuwa wakivuka ziwa, Yesu akalala usingizi. Mara moja zoruba kali ikaanza kuvuma, hata maji yakaanza kuingia ndani ya chombo, nao wakakuwa katika hatari.
Nami ninafurahi kwa ajili yenu, kwa sababu sikukuwa kule, kusudi mupate kuamini. Tuende kule anapokuwa.”