19 Mwalimu mumoja wa Sheria akamufikia na kumwambia: “Mwalimu, nitakufuata popote utakapokwenda.”
Ezra akaondoka Babeli, yeye alikuwa mwandishi mwenye ujuzi mwingi sana katika Sheria ambayo Yawe, Mungu wa Israeli, alikuwa amemupatia Musa. Na kwa musaada wa Yawe, Mungu wake, mufalme alimupatia Ezra kila kitu alichohitaji.
Ni vile inavyokuwa, hakuna mumoja wenu atakayeweza kuwa mwanafunzi wangu kama asipoacha vyote anavyokuwa navyo.”
Basi, tuseme nini juu ya wenye hekima, walimu wa Sheria, nao wafundi wa usemi siku hizi? Mungu ameonyesha wazi kwamba hekima ya dunia hii ni upumbafu!
Labda nitabakia pamoja nanyi muda kidogo, au tena wakati wote wa mvua kali; kusudi muweze kunisaidia kuendelea pahali popote nitakapokwenda.