Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 8:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Na ilipokuwa magaribi, wakamuletea Yesu watu wengi waliokuwa na pepo. Naye akawafukuza wale pepo akiwaamuru kwa neno tu na kuwaponyesha wagonjwa wote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 8:16
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

akawaambia: “Ikiwa mutaisikiliza kwa uaminifu sauti yangu mimi Yawe, Mungu wenu, kutenda yale yanayokuwa sawa mbele yangu, na kuheshimu amri na masharti yangu yote, basi, mimi sitawaletea yale magonjwa niliyowaletea Wamisri. Kwa sababu, mimi ni Yawe ninayewaponya ninyi.”


Kisha wakamuletea Yesu mutu mumoja aliyeshikwa na pepo, aliyemufanya kuwa kipofu na bubu. Yesu akamuponyesha mutu yule hata akaanza kusema na kuona.


Yesu alipotoka ndani ya chombo, akaona kundi kubwa la watu, naye akawasikilia huruma, akawaponyesha wale waliokuwa wagonjwa kati yao.


Yesu akamugusa mukono, naye akapona homa. Halafu mama yule akasimama na kuanza kumushugulikia.


Wachungaji wa nguruwe wale wakaenda mbio katika muji kupasha habari za mambo yaliyotendeka na habari ya wale watu wawili waliokuwa na pepo.


Na kule wakamuletea mutu mwenye ugonjwa wa kupooza, akilala juu ya kipoyi. Yesu alipoona namna watu wale walivyomwaminia, akamwambia yule mwenye kupooza: “Mutoto wangu, ujipe moyo! Zambi zako zimesamehewa!”


wakamuletea mugonjwa mwenye kupooza, akibebwa na watu wane.


(Alisema hivi kwa sababu Yesu alikuwa akimwamuru: “Wewe pepo, toka ndani ya mutu huyu!”)


Wakati Yesu alipoona watu wengi wanazidi kukusanyika mbiombio, akamukaripia yule pepo na kumwambia: “Wewe pepo wa bubu na wa kiziwi, ninakuamuru utoke ndani ya mutu huyu wala usimurudilie tena!”


Yesu alipomwona yule mwanamuke, akamwita, akamwambia: “Ewe mama, ugonjwa wako umepona.”


Jua lilipotua, wakamuletea Yesu watu wote wenye kuwa na magonjwa mbalimbali. Akaweka mikono yake juu ya kila mumoja wao, akawaponyesha.


Pepo wakatoka ndani ya watu wengi, wakilalamika, wakisema: “Wewe ni Mwana wa Mungu!” Lakini Yesu akawakaripia, na hakuwaachilia waseme neno, kwa sababu walijua kwamba yeye ndiye Kristo.


Na kufuatana na mambo yote yaliyotokea, watu waliwapeleka wagonjwa katika barabara, wakiwalalisha juu ya mikeka na vipoyi kusudi Petro atakapopita, kivuli chake kipate tu kufika kwenye wamoja wao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ