Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 8:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Yesu akamugusa mukono, naye akapona homa. Halafu mama yule akasimama na kuanza kumushugulikia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 8:15
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku moja, wakati wa mazishi, watu waliona moja kati ya makundi yale. Wakatupa maiti katika kaburi la Elisha na kukimbia. Mara tu maiti hiyo ilipogusa mifupa ya Elisha, ilifufuka na kusimama wima.


Naye akinigusa nalo kwenye mudomo, akasema: Kaa hili limekugusa kwenye mudomo; umeondolewa kosa lako, umesamehewa zambi yako.


na kumusihi awaruhusu waguse hata upindo wa nguo yake tu. Nao wote waliougusa walipona.


Yesu akawasikilia huruma. Akagusa macho yao, na mara moja wakapata kuona, nao wakamufuata.


Kisha Yesu akafika kwa nyumba ya Petro, na mule akamukuta mama mukwe wa Petro amelala katika kitanda na ugonjwa wa homa.


Na ilipokuwa magaribi, wakamuletea Yesu watu wengi waliokuwa na pepo. Naye akawafukuza wale pepo akiwaamuru kwa neno tu na kuwaponyesha wagonjwa wote.


Yesu akanyoosha mukono, akamugusa na kumwambia: “Ninataka, utakaswe!” Na mara moja mutu yule akatakaswa ukoma wake.


Na kulikuwa mwanamuke mumoja mwenye ugonjwa wa kutokwa na damu kwa muda wa miaka kumi na miwili. Yeye akakuja nyuma ya Yesu na kugusa upindo wa nguo yake,


Halafu Yesu akagusa macho yao, akisema: “Ifanyike kwenu sawa vile munavyoaminia.”


Yesu na wanafunzi wake walipotoka ndani ya ile nyumba ya kuabudia, mara moja wakaenda kwa nyumba ya Simoni na Andrea, wakiwa pamoja na Yakobo na Yoane.


Yesu akamusikilia huruma, akanyoosha mukono, akamugusa na kumwambia: “Ninataka utakaswe!”


Lakini Yesu akamushika mukono na kumwambia kwa sauti kubwa: “Mutoto, simama!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ