Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 7:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 “Muombe, nanyi mutapewa; mutafute, nanyi mutapata; mupige hodi, nanyi mutafunguliwa mulango.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 7:7
43 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku ileile watumishi wa Isaka walimufikia na kumupasha habari za kile kisima walichokuwa wamechimba, wakasema: “Tumepata maji!”


Kule Gibeoni, Yawe alimutokea Solomono katika ndoto usiku, akamwambia: “Omba kitu chochote unachotaka nami nitakupa.”


Ee Yawe, unapokea maombi ya muzaifu; unamutia moyo na kumutegea sikio.


Katika majivuno yake anasema: “Mungu hatagundua. Hakuna Mungu.” Hayo ndiyo mawazo yake yote.


Utukuzwe, ee Yawe! Unifundishe masharti yako.


Moyo wangu unaniambia: “Kuja umutafute Mungu!” Basi, ninakutafuta, ee Yawe.


Mumutukuze Yawe pamoja nami, wote pamoja tulisifu jina lake.


Uitafute furaha yako kwa Yawe, naye atakujalia unayotamani katika moyo.


Uniite wakati wa taabu, nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”


Jambo hili litamupendeza Yawe zaidi, kuliko kumutolea sadaka ya ngombe, kuliko kumutolea ngombe dume muzima.


Wapumbazike kwa haya, hao wanaofurahia kunizomea!


Ee Bwana, wewe ni muzuri na mwenye kusamehe, mwingi wa wema kwa wote wanaokuomba.


Ninawapenda wale wanaonipenda; wanaonitafuta kwa bidii wananipata.


Nikaamuka, nikazunguka katika muji, katika barabara na nafasi za makutano, nikimutafuta yule wangu wa moyo. Nilimutafuta, lakini sikumupata.


Enyi watu wa Sayuni, enyi watu wa Yerusalema, hakika ninyi hamutaomboleza tena. Kweli Mungu atawahurumia; mara tu atakaposikia kilio chenu atawaitikia.


Uniite, nami nitakujibu na kukuambia mambo makubwa yaliyofichwa ambayo haujapata kuyajua.


Yawe anawaambia Waisraeli hivi: Munitafute mimi nanyi mutaishi!


“Kweli ninawaambia tena: wawili kati yenu hapa katika dunia wakipatana kwa kuomba juu ya kitu chochote, Baba yangu anayekuwa mbinguni atawapa kitu kile.


Na kitu chochote mutakachoomba, mukiamini, mutakipata.”


Lakini ninyi mushugulikie kwanza Ufalme wa Mungu na kufuata haki mbele yake, naye atawaongezea vitu vile vyote.


Basi ikiwa ninyi munaokuwa waovu munajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, zaidi sana Baba yenu anayekuwa mbinguni atawapa wale wanaomwomba vitu vizuri zaidi.


Kwa maana kila mutu anayeomba, anapewa; naye anayetafuta, anapata, naye anayepiga hodi, anafunguliwa.


Ni kwa hiyo ninawaambia kwamba munapoomba kwa ajili ya hitaji la kitu fulani, mwamini kama mumekwisha kukipokea, na kwa njia hiyo mutakipewa.


“Mwenye nyumba atakapokwisha kusimama na kufunga mulango, ninyi mutabaki inje na kuanza kupiga hodi na kusema: ‘Bwana, utufungulie.’ Naye atawajibu: ‘Sijui munatokea wapi.’


Halafu Yesu akawaambia wanafunzi wake mufano huu kwa kuwaonyesha kwamba wanapaswa kuomba siku zote pasipo kuchoka.


Ninyi hamukunichagua mimi, lakini ni mimi niliyewachagua ninyi. Nami nimewatuma muende kuzaa matunda yasiyokuwa na mwisho. Kwa hiyo Baba atawapa chochote munachoomba kwa jina langu.


Kama mukikaa ndani yangu na maneno yangu yanakaa ndani yenu, mutaomba chochote munachotaka, nanyi mutakipewa.


Yesu akamujibu: “Kama ungejua kitu Mungu anachoweza kukupatia, na ni nani anayekuomba maji ya kunywa, wewe ndiwe ungemwomba, naye angekupa maji ya uzima.”


Wale wanaofanya matendo mema bila kuchoka na kutafuta toka kwa Mungu utukufu, heshima na uzima usiokuwa na mwisho, Mungu atawapa uzima wa milele.


Hakuna mutu mwenye ufahamu, hakuna mwenye kushugulika na Mungu.


Basi pasipo imani, hakuna mutu anayeweza kumupendeza Mungu. Kwa maana mutu anayetaka kumwendea Mungu sherti aamini kwamba Mungu yuko, na kwamba anawapa zawadi wale wanaomutafuta.


Nao wakiomba kwa imani, mugonjwa yule atapona, kwa kuwa Bwana atamurudishia afya yake. Na ikiwa amefanya zambi, atasamehewa.


Nasi tunapokea jambo lolote tunaloomba kwake, kwa sababu tunatii amri zake na kutenda mambo yanayomupendeza.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ