Wewe munafiki, ondosha kwanza nguzo kutoka ndani ya jicho lako, kisha utaweza kuona waziwazi na kuweza kuondoa ile vumbi inayokuwa ndani ya jicho la ndugu yako.
Katika safari zangu nyingi nimepata hatari ya mafuriko ya mito, hatari ya wanyanganyi, hatari kutoka kwa wanainchi wenzangu na kutoka kwa watu wa mataifa mengine. Nilikuwa katika hatari ndani ya miji, katika jangwa, katika bahari na kati ya wandugu za uongo.
Basi munazania itakuwa namna gani? Hataazibiwa vikali zaidi yule anayemuzarau Mwana wa Mungu na kuihesabu kuwa bure damu ya agano la Mungu iliyomutakasa na kumutukana Roho wa neema?
kisha wakianguka, haiwezekani kuwarudisha hata wapate kugeuka mara ingine toka katika matendo yao mabaya. Kwa sababu wamemutundika wao wenyewe Mwana wa Mungu mara ya pili na kumupatisha haya mbele ya watu.