Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 7:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Kwa maana mutahukumiwa kufuatana na namna munavyowahukumu wengine, na kipimo kile munachowapimia wengine ndicho kitakachotumiwa kwenu vilevile.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 7:2
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wao wakamwambia mufalme: “Saulo alikusudia kutuua sisi na kutuangamiza kusipate kubakia mutu yeyote wetu popote katika eneo lolote la Israeli.


Yeye alipenda kulaani watu; laana imupate yeye mwenyewe. Hakuwatakia wengine baraka; basi, asipate baraka yeye mwenyewe.


jicho kwa jicho, jino kwa jino, mukono kwa mukono, muguu kwa muguu,


Ole kwako! Unaangamiza ingawa hauangamizwi. Unadanganya ingawa haudanganywi. Utakapokwisha kuangamiza, wewe utaangamizwa! Utakapomaliza kudanganya, wewe utadanganywa.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Ninyi hamukunitii juu ya kuwapatia wandugu zenu Waisraeli uhuru. Basi, nami vilevile nitawapatia ninyi uhuru: uhuru wa kuuawa kwa upanga katika vita, kuuawa kwa ugonjwa mukali na kwa njaa. Nitawafanya ninyi kuwa kitambulisho cha kuogopesha kwa falme zote katika dunia.


Nitaiazibu Babeli na wakaaji wote wa Kaldea mukiona kwa macho yenu wenyewe, kwa sababu ya uovu wote walioufanya katika Sayuni. –Ni ujumbe wa Yawe.


Siku inakaribia ambapo mimi Yawe nitayahukumu mataifa yote. Kama vile mulivyowatendea wengine, ndivyo mutakavyotendewa, mutalipwa kulingana na matendo yenu.


“Hivi, mukiwasamehe watu wengine makosa wanayowatendea, Baba yenu anayekuwa mbinguni atawasamehe vilevile.


Yesu akawaambia tena: “Muangalie vizuri maneno munayosikia! Mungu atawapimia na kipimo kile munachowapimia wengine, na kuwaongezea hata zaidi.


Muwape wengine, na Mungu atawapa ninyi. Mutapokea kipimo kikubwa kilichojaa zaidi. Kwa maana mutapimiwa na kipimo kile munachotumia kwa wengine.”


Mukumbuke maneno haya: yule anayepanda kidogo atavuna kidogo, na yule anayepanda kwa uwingi atavuna kwa uwingi.


Kwa sababu Mungu hatahurumia mutu yule asiyehurumia wengine. Lakini huruma ya Mungu itaishinda hukumu.


Mutendee muji ule sawa vile ulivyowatendea. Mulipize matendo yake mara mbili zaidi. Na katika kile kikombe alimochanganya divai yake, mumuchangie divai inayokuwa kali mara mbili zaidi kuliko ile aliyowapa.


Adoni-Bezeki akasema: “Wafalme makumi saba waliokatwa vidole gumba vya mikono na miguu waliokota makombo chini ya meza yangu. Sasa Mungu amenilipa kama nilivyotenda.” Wakamupeleka Yerusalema, akakufia kule.


Sisera akainama, akaanguka; akalala kimya kwenye miguu yake. Hapo alipoinama ndipo alipoanguka amekufa!


Samweli akasema: “Kwa sababu upanga wako umewafanya wamama wengi wasikuwe na watoto, ndivyo na mama yako atakavyokuwa bila mutoto kati ya wamama.” Akamukatakata Agagi vipandevipande mbele ya Yawe kule Gilgali.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ