Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 7:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Basi ikiwa ninyi munaokuwa waovu munajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, zaidi sana Baba yenu anayekuwa mbinguni atawapa wale wanaomwomba vitu vizuri zaidi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 7:11
35 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe alipoona uwingi wa uovu wa watu katika dunia, na kwamba kila kitu mwanadamu anachokusudia ndani ya moyo wake ni kiovu siku zote,


Harufu nzuri ya sadaka hiyo ikamupendeza Yawe, naye akasema ndani ya moyo wake: “Sitailaani tena inchi hata kidogo kwa sababu ya mwanadamu. Ninajua kwamba mawazo yake ni maovu tangu utoto wake. Wala sitaangamiza tena viumbe vyote kama vile nilivyofanya.


Tena jambo hili lilikuwa dogo mbele ya macho yako. Zaidi ya hayo, Bwana wangu Yawe, umeahidi kuchunga jamaa yangu kwa miaka mingi inayokuja na kunijulisha hivyo, ee Bwana wangu Yawe.


kefu sasa mwanadamu anayekuwa chukizo na mupotovu, mwanadamu anayetenda uovu kama kunywa maji!


Siku moja tu ndani ya hekalu lako, ni bora kuliko siku elfu pahali pengine; afazali kubakia kwa mulango wa nyumba yako, kuliko kuishi ndani ya nyumba ya waovu.


Uaminifu utachipuka katika inchi; haki utashuka toka mbinguni.


Lakini wewe, Bwana, ni Mungu wa rehema na huruma; wewe ni muvumilivu, mwingi wa wema na uaminifu.


Ee Bwana, wewe ni muzuri na mwenye kusamehe, mwingi wa wema kwa wote wanaokuomba.


Lakini Yawe anasema: Munafikiri kwamba mama anaweza kumusahau mutoto anayemunyonyesha, wala kumuchukia mutoto wa tumbo lake? Hata kama mama anaweza kumusahau mutoto wake, mimi sitakusahau hata kidogo.


Nitakumbusha mema ya Yawe, sifa za Yawe, matendo yake yote kwetu, mambo mazuri aliyowatendea Waisraeli, rehema yake, na wingi wa wema wake.


Moyo wa mutu ni mudanganyifu kuliko vitu vyote; hauwezi kuponyeshwa, hakuna anayeweza kuuelewa!


Siku zinakuja ambapo nitatimiza ahadi yangu niliyofanya na Waisraeli na Wayuda.


Enyi Waisraeli, mumurudilie Yawe, Mungu wenu. Mumejikwaa kwa sababu ya uovu wenu.


Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe? Wewe unasemehe zambi za watu wako waliobaki, wala hauyaangalii makosa yao. Hasira yako haidumu milele, lakini unapendelea zaidi kutuonyesha wema wako.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mutoto anamuheshimu muzazi wake, na mutumishi anamuheshimu bwana wake. Ikiwa mimi ndiye Baba wenu, mbona munanivunjia heshima? Ikiwa mimi ni bwana wenu, mbona hamuniheshimu? Ninasema hivyo kwa ninyi makuhani munaozarau jina langu. Nanyi munauliza: Sisi tumezarau jina lako namna gani?


Vilevile hapa katika dunia musimwite mutu yeyote ‘Baba’ kwa maana muko na Baba mumoja tu, anayekuwa mbinguni.


Au nani anaweza kumupa nyoka kama akimwomba samaki?


Kwa maana Mungu alipenda sana ulimwengu hata kumutoa Mwana wake wa pekee, kusudi kila mutu anayemwamini asipotee, lakini apate uzima wa milele.


Basi tunajua kama maneno yote yanayosemwa na Sheria, yanawaelekea wale wanaolazimishwa kutii Sheria, kusudi mutu yeyote asikuwe na namna ya kujitetea, na dunia nzima ipaswe kuhukumiwa na Mungu.


Basi tuseme nini? Sisi Wayuda tunawapita watu wa mataifa mengine nini? Hatuwapiti kitu hata kimoja! Kwa maana nimekwisha kuonyesha kwamba Wayuda na watu wa mataifa mengine wote wako chini ya utawala wa zambi.


Yeye hakumwacha Mwana wake wa pekee, lakini alimutoa kwa ajili yetu sisi wote. Namna gani atakosa kutupatia vilevile vitu vyote kwa njia ya mwana wake?


Lakini Maandiko Matakatifu yanasema kwamba watu wote wako chini ya utumwa wa zambi, kusudi zawadi iliyoahidiwa na Mungu itolewe kwa wale wanaoamini kwa njia ya imani yao katika Yesu Kristo.


Kila zawadi nzuri na kila zawadi kamilifu inatoka juu kwa Mungu Baba aliyeumba miangaza yote inayokuwa katika mbingu. Mungu hawezi kubadilika wala kugeuka.


Muangalie namna Baba alivyoonyesha upendo wake kwetu hata tupate kuitwa watoto wa Mungu! Na kwa hakika sisi ndio wao! Ndiyo maana watu wa dunia hawatutambui, kwa sababu hawakumujua Mungu.


Na huu ndio upendo: si kwamba sisi tulimupenda Mungu, lakini kwamba ni yeye ndiye aliyetupenda hata akatuma Mwana wake kama vile sadaka iliyotolewa kwa ajili ya usamehe wa zambi zetu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ