Matayo 6:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
23 Lakini kama macho yako yanaharibika, mwili wako wote utabaki katika giza. Basi ikiwa mwangaza unaokuwa ndani yako umegeuka kuwa giza, giza hilo ni nzito sana!
Yawe anasema: Watu wangu ni wapumbafu, hawanijui mimi. Wao ni watoto wajinga; hawana ufahamu. Wao wanaelewa vizuri kutenda maovu, lakini hawajui kutenda mema.
Jicho ni taa ya mwili. Kama jicho lako likiwa zima, mwili wako wote utabaki katika mwangaza. Lakini kama jicho lako linaharibika, mwili wako vilevile utabaki katika giza.
Akawajibu: “Ninyi mumefunuliwa kujua siri ya Ufalme wa Mungu, lakini kwa watu wengine si vile. Wao wanaambiwa maneno hayo kwa njia ya mifano, kusudi waangalie, lakini wasione kitu, nao wasikie, lakini wasifahamu kitu.”
Lakini mutu anayefuata hali yake ya kidunia hawezi kukubali maneno yanayotoka kwa Roho yule. Kwa sababu anayaona kuwa ni upumbafu kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa maana yanatambulikana tu kwa njia ya Roho.
na wenye mafikiri yaliyotiwa katika giza. Watu hawa hawashiriki katika uzima ule unaoletwa na Mungu, kwa sababu wao ni wapumbafu na wenye mioyo migumu.