Lakini macho yako wewe na moyo wako, vinaelekea tu mapato yasiyokuwa ya haki. Unamwanga damu ya wasiokuwa na kosa, nawe unawatesa watu na kuwatendea kwa ukali.
Maana sisi hatuangalii vitu vile vinavyoonekana, lakini vitu visivyoonekana. Kwa sababu vile vinavyoonekana vinadumu muda kidogo tu, lakini vile visivyoonekana, vinadumu milele.
Basi wandugu zangu, muangalie vizuri, kati yenu kusikuwe mutu mumoja mwenye moyo mubaya wa kutokuamini, aliyefikia hata kujitenga mbali na Mungu Mwenye Uzima.