Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 6:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 “Musijiwekee akiba katika dunia hii, pahali nondo na kutu vinapoharibu, nao wizi wanapotoboa nyumba na kuiba.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 6:19
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Usiku wezi wanavunja nyumba, lakini muchana wanajifungia ndani; wala hawajui kabisa mwangaza ni nini.


Sikuweka tumaini langu katika zahabu, sikuiambia zahabu safi: “Wewe ni usalama wangu”,


Kumbe umenipimia maisha mafupi sana! Maisha yangu si kitu mbele yako. Hakika, kila mwanadamu ni kama pumzi tu!


Wanadamu wote ni kama pumzi tu; wote, wakubwa kwa wadogo, hawafai kitu. Wakipimwa wote pamoja, pumzi ni nzito kuliko wao.


Lakini mwizi akishikwa wakati jua limechomoza na kuuawa, aliyemwua atakuwa na kosa. Mwizi anapaswa kulipa. Ikiwa hana kitu cha kulipa, basi, yeye mwenyewe atauzishwa kwa kulipa kile alichoiba.


Utajiri haufai kitu siku ya kasirani, lakini haki inaokoa kutoka kifo.


Kupata hekima ni bora kuliko zahabu; kupata akili ni chaguo bora kuliko feza.


Mungu anamujalia mutu anayependezwa naye hekima, akili na furaha; lakini anamupa mwenye zambi kazi ya kuvuna na kulundika, kisha Mungu anavipatia yule anayemupendeza. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Feza yao wala zahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya kasirani ya Yawe. Kwa moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa. Kwa ukamilifu na kwa namna ya kuogopesha atawafanya wakaaji wote katika dunia watoweke.


Yesu akamujibu: “Ukitaka kuwa mutimilifu, kwenda uuzishe vitu unavyokuwa navyo, na uwape wamasikini mali zile, nawe utakuwa na akiba mbinguni. Kisha urudi, unifuate.”


Lakini mujiwekee akiba katika mbingu, pahali nondo wala kutu visipoweza kuharibu, nao wizi wasipoweza kutoboa na kuiba.


Yesu akaongeza kusema: “Ni hivi inavyokuwa kwa yule anayejiwekea mali mengi, lakini mbele ya Mungu hahesabiwi kuwa na kitu.”


Muuzishe vitu munavyokuwa navyo, muwasaidie wamasikini. Mujiwekee feza zisizoweza kuwa na upungufu, nayo akiba isiyoweza kumalizika katika mbingu. Kule wizi hawawezi kukaribia wala nondo hawaharibu.


Munajua vema kwamba mwenye nyumba angejua saa gani mwizi atakapokuja kumwiba, asingeacha nyumba yake ibomolewe.


Yesu aliposikia maneno haya, akamwambia: “Ungali unakosewa na kitu kimoja tu: uuzishe vitu vyote unavyokuwa navyo, na uwape wamasikini mali zile, nawe utakuwa na akiba mbinguni. Kisha urudie unifuate!”


Yesu alipoona kwamba amehuzunika sana, akasema: “Kweli ni vigumu sana kwa watajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu,


Uwaagize wale wanaokuwa watajiri katika dunia hii ya sasa wasijivune, vilevile wasiweke matumaini yao katika mali inayotoweka upesi. Lakini wamutumainie Mungu anayetupatia vitu vyote kwa uwingi kusudi tufurahiwe navyo.


Musijiachilie kutawaliwa na tamaa ya mali katika maisha yenu, lakini mutoshelewe na vitu munavyokuwa navyo, kwa maana Mungu mwenyewe amesema: “Sitakusahau wala kukuachilia.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ