Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 6:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 “Munapofunga kula chakula, musifanye kama wanafiki, wanaojigeuza kuwa wenye sikitiko na kukunja nyuso zao, kusudi watu waone kwamba wanafunga. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 6:16
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Daudi alimwomba Mungu kwa ajili ya mutoto yule. Akafunga kula chakula, akaingia ndani ya chumba chake, na usiku kucha akalala chini.


Halafu watumishi wake wakamwuliza: “Ni jambo gani hili ulilofanya? Mutoto alipokuwa muzima, wewe ulifunga na kumulilia. Lakini alipokufa, ukasimama, ukakula chakula.”


Lakini, Ahabu aliposikia maneno hayo, akapasua nguo zake, akavaa gunia peke yake, akafunga, akakuwa analala na gunia, na kwenda huko na huko kwa huzuni.


Niliposikia hayo nikaikaa chini na kulia, nikaomboleza kwa siku za kutosha. Nikafunga kula na kumwomba Mungu wa mbinguni,


“Kwenda uwakusanye pamoja Wayuda wote wanaokuwa katika muji wa Susani. Mufunge, musikule wala musikunywe kwa siku tatu, usiku na muchana, kwa ajili yangu. Na mimi na wajakazi wangu tutafanya vile vile. Kisha, nitamwendea mufalme, ingawa ni kinyume cha sheria. Kama ni kuuawa, niuawe.”


Magoti yangu yanaregea kwa ajili ya kufunga kula chakula; nimebaki mifupa na ngozi.


Lakini wao walipokuwa wagonjwa, mimi nilivaa magunia kuonyesha huzuni, nilijitesa kwa kufunga kula chakula. Niliomba nikikuwa nimeinamisha kichwa.


Upendo wangu kwa ajili ya nyumba yako unanichoma. Matusi wanayokutukana yananiangukia.


Nilimwomba Yawe, kwa moyo, nikimutolea maombi pamoja na kufunga kula chakula, nikavaa gunia na kuikaa kwenye majivu.


Ninyi mumesema: Kumutumikia Mungu hakuna faida. Kuna faida gani kuyatii maagizo ya Yawe wa majeshi, au kujaribu kumwonyesha kwamba tumekosa mbele yake kwa kutembea kama watu wanaoomboleza?


“Mujiangalie musifanye matendo mema mbele ya watu kusudi mujionyeshe kwao. Kwa maana mukifanya hivi hamutapata faida kutoka kwa Baba yenu anayekuwa mbinguni.


“Basi wakati unapomusaidia masikini, usipige baragumu, kama vile wanafiki wanavyofanya katika nyumba za kuabudia na katika barabara kusudi wasifiwe na watu. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.


“Munapoomba, musikuwe kama wanafiki, kwa maana wanapenda kuomba wakisimama katika nyumba za kuabudia na pembeni ya barabara, kusudi wapate kujionyesha mbele ya watu. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.


Wanafunzi wa Yoane Mubatizaji na Wafarisayo walikuwa wakifunga kula chakula. Hivi watu wakakuja kumwuliza Yesu: “Sababu gani wanafunzi wa Yoane Mubatizaji na wanafunzi wa Wafarisayo wanafunga kula chakula, lakini wanafunzi wako hawafungi?”


Ninafunga kula chakula mara mbili kila juma na ninatoa fungu moja la kumi la vitu vyote ninavyopata.’


Kisha akabaki mujane, hata akaeneza umri wa miaka makumi nane na mine. Alibaki katika hekalu, akitumikia Mungu usiku na muchana, akifunga kula chakula na kuomba.


Kornelio akajibu: “Kumekwisha kupita siku tatu, mimi nilikuwa nikiomba ndani ya nyumba yangu kwa saa hii hii ya saa tisa ya muchana. Mara moja nikaona mutu anayevaa nguo yenye kungaa sana, akisimama mbele yangu.


Wakawachagua wazee katika kila kanisa. Na kisha kuomba na kufunga kula chakula, wakawaweka chini ya ulinzi wa Bwana waliyemwamini.


Musinyimane, isipokuwa tu mumepatana na kwa muda tu kusudi mupate wakati wa kujitoa kwa kufunga na kuomba. Kisha munaweza kurudiliana tena kusudi Shetani asiwajaribu katika uzaifu wenu.


Nimesumbuka kwa kufanya kazi ngumu, nimepata magumu, nimekesha mara nyingi. Mara nyingi niliteswa na njaa na kiu; mara nyingi nililazimishwa kutokula. Nimeteseka na baridi na ukosefu wa nguo.


Tumepigwa, tumetiwa ndani ya kifungo, wamefanya fujo juu yetu, tumefanya kazi ngumu, tumekoseshwa usingizi na kukaa bila kula.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ