Usikilize wakati tunapokusihi, mimi mutumishi wako na watu wako Waisraeli ambao tutaomba tukielekea pahali hapa. Kutokea kwako mbinguni, usikilize. Na ukisha kusikiliza, utusamehe.
basi, usikilize kule kwako mbinguni, uwasamehe na kumutendea kila mutu kwa kadiri anavyostahili, maana ni wewe tu unayejua mawazo ya mioyo ya wanadamu wote,
Anawatendea mema maelfu, anawasamehe uovu, makosa na zambi. Lakini hataacha kumwazibu mwenye kosa. Anawalipiza watoto na wajukuu uovu wa baba na babu zao, hata kizazi cha tatu na cha ine.
Ee Yawe, utusikie; utusamehe ee Yawe. Ee Yawe, kwa ajili ya heshima yako utusikie na utende, wala usikawie, ee Mungu wangu, kwa ajili ya muji huu na watu hawa wanaoitwa kwa jina lako!
Na kule wakamuletea mutu mwenye ugonjwa wa kupooza, akilala juu ya kipoyi. Yesu alipoona namna watu wale walivyomwaminia, akamwambia yule mwenye kupooza: “Mutoto wangu, ujipe moyo! Zambi zako zimesamehewa!”
Vilevile munazani kwamba wale watu kumi na wanane waliokufa munara ulipowaangukia kule Siloamu, walikuwa wakosaji kuliko wakaaji wengine wote wa Yerusalema?
“Musiwahukumu wengine, na Mungu hatawahukumu ninyi. Musikuwe wenye kukatia wengine azabu, naye hatawaazibu ninyi. Muwasamehe wengine, na Mungu atawasamehe ninyi vilevile.
“Basi wandugu zangu, mujue hakika kwamba kwa njia ya huyo, habari ya kusamehewa zambi inahubiriwa kwenu. Na zaidi ya hii, hakuna mutu anayeweza kuhesabiwa haki katika mambo yote kwa njia ya kushika Sheria ya Musa. Lakini kila mutu anayemwamini anahesabiwa haki katika mambo yale.
Muvumiliane na kusameheana ninyi kwa ninyi wakati wowote mutu anapokuwa na neno la kumushitaki mwingine. Munapaswa kusameheana kama vile Bwana alivyowasamehe ninyi.