Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 6:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Ufalme wako ukuje; mapenzi yako yafanyike katika dunia kama inavyokuwa mbinguni.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 6:10
44 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ezra akaomba akisema: Wewe peke yako ndiwe Yawe! Ulifanya mbingu na jeshi lake lote, dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake, bahari na vyote vinavyokuwa ndani yake. Unavipatia uzima, na jeshi lote la mbinguni linakuabudu wewe.


“Nimemusimika mufalme niliyemuchagua; anatawala Sayuni, mulima wangu mutakatifu!”


Halafu nikasema: “Ninakuja. Katika kitabu imeandikwa juu yangu.


Katika siku zinazokuja, itatukia kwamba mulima wa nyumba ya Yawe utaimarishwa kupita milima yote, utainuliwa juu ya vilima vyote. Mataifa yote yatajaa kule,


Siku zinakuja ambapo nitaotesha kichipukizi cha haki toka kizazi cha Daudi. Huyo atatawala kama mufalme, atatenda kwa hekima naye ataimarisha sheria yangu na haki katika inchi.


Wakati wa wafalme wale, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaangamizwa hata kidogo. Watu wengine hawataushinda na kuutawala ufalme huo, lakini ufalme huo utaziponda na kuzikomesha falme zilizotangulia, nao utadumu milele.


Wakati wa maono haya usiku, niliona kiumbe kinachofanana na mwanadamu. Akakuja katika mawingu na kumwendea yule Muzee wa zamani sana. Akakaribishwa mbele yake.


Ufalme, utawala na ukubwa wa falme zote katika dunia watapewa kwa watu wa watakatifu wa Mungu Mukubwa. Ufalme wao utakuwa wa kudumu milele, na tawala zote zitawatumikia na kuwatii.


Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.


Kwa maana yeyote anayefanya mapenzi ya Baba yangu anayekuwa katika mbingu, huyu ndiye ndugu yangu, dada yangu na mama yangu.”


Kweli ninawaambia: wamoja kati ya watu wanaokuwa hapa hawatakufa mbele hawajamwona Mwana wa Mutu akikuja katika Ufalme wake.”


Akawaacha tena kwa mara ya pili, akaomba akisema: “Ee Baba yangu, kama kikombe hiki cha mateso hakiwezi kupita mbali nami, bila mimi kukikunywa, basi mapenzi yako yafanyike!”


akisema: “Mugeuke toka zambi zenu, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia!”


Tangia wakati huo Yesu akaanza kuhubiri, akisema: “Mugeuke toka zambi zenu, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia!”


“Si kila mutu anayeniita ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa mbinguni, lakini yule tu anayefanya mapenzi ya Baba yangu anayekuwa mbinguni.


Ubarikiwe ufalme unaokuja, ndio ufalme wa babu yetu Daudi! Mungu asifiwe juu mbinguni!”


Kwa sababu mutu yeyote anayefanya mapenzi ya Mungu, huyu ndiye ndugu yangu, dada yangu na mama yangu.”


Watu walipokuwa wakisikiliza maneno hayo, Yesu akaongeza kuwaambia mufano mumoja, kwa sababu alikuwa karibu na muji Yerusalema, na watu wale walizani kwamba siku za Ufalme wa Mungu zitafika saa ile ile.


Wakasema: “Abarikiwe mufalme anayekuja kwa jina la Bwana! Amani mbinguni na utukufu kwa Mungu anayekuwa juu!”


“Baba, kama ukitaka, ninakuomba uniondolee mbali kikombe cha mateso. Lakini isikuwe mapenzi yangu ndiyo yafanyike, lakini yako.” [


Yesu akawaambia: “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya yule aliyenituma na kutimiza kazi yake.


Hakika mapenzi ya Baba yangu ni kwamba kila mutu anayemwona Mwana na kumwamini apate uzima wa milele, nami nitamufufua siku ya mwisho.”


Kama mutu akitaka kufanya mapenzi ya Mungu, atajua kama mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu, au kama ninasema kwa mamlaka yangu mwenyewe.


Kisha kumwondosha Saulo, Mungu akasimika Daudi kuwa mufalme wao. Na yeye mwenyewe alimushuhudia akisema: ‘Nimejichagulia Daudi mwana wa Yese, kwa maana ni mutu mwenye kunipendeza. Huyu ndiye atakayefanya mambo yote ninayotaka.’


Tulipoona kwamba amekataa shauri letu, tukanyamaza na kusema: “Mapenzi ya Bwana yafanyike.”


Kisha akasema: ‘Mungu wa babu zetu amekwisha kukuchagua wewe kusudi ujue mapenzi yake. Anataka umwone Mwenye Haki, na kumusikia akisema kwa kinywa chake mwenyewe.


Musifuate mwenendo wa siku hizi, lakini muache Mungu awabadilishe kwa kugeuza upya nia zenu, hata mukuwe na mawazo mapya. Kwa hiyo mutaweza kutambua mapenzi ya Mungu. Mutajua mambo gani yanayokuwa mema, yanayomupendeza Mungu na yanayokuwa makamilifu.


Musitumike tu wakati wanapowaangalia, mukitafuta kuwapendeza. Lakini mutimize mapenzi ya Mungu kwa moyo wote mukijihesabu kama watumwa wa Kristo.


Kwa maana yeye ametuokoa toka katika uwezo wa giza, na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wake mupendwa,


Kwa sababu hii hatuchoki kuwaombea ninyi, tangu siku tuliposikia habari zenu. Tunamwomba Mungu awawezeshe kujua kabisa mapenzi yake na kuwajaza hekima na akili inayotoka kwa Roho wake.


Kitu Mungu anachotaka ni kwamba mukuwe watakatifu na muepuke mambo ya uasherati.


Mumushukuru Mungu katika mambo yote. Kwa maana hayo ndiyo mambo Mungu anayotaka mufanye katika kuungana kwenu na Yesu Kristo.


Malaika ni nini, basi? Wao wote ni roho wanaomutumikia Mungu na wanaotumwa naye kwa ajili ya faida ya wale wanaopaswa kuokolewa.


Munapaswa kuvumilia, kusudi mutimize mapenzi ya Mungu, na kuweza hivi kupewa kile mulichoahidiwa.


Halafu nikasema: ‘Niko hapa, ee Mungu, nimekuja kufanya mapenzi yako, kama ilivyoandikwa juu yangu katika kitabu cha Sheria.’ ”


awakamilishe katika kila tendo jema kusudi mupate kutimiza mapenzi yake; yeye atimize ndani yetu yale yanayomupendeza, kwa njia ya Yesu Kristo. Yesu atukuzwe milele na milele. Amina.


Na hayo ndiyo mapenzi ya Mungu, anayetaka munyamazishe usemi wa ujinga wa wapumbafu kwa njia ya kutenda mema.


Sasa, musiishi tena kufuatana na tamaa za kimutu, lakini muishi kufuatana na mapenzi ya Mungu kwa muda unaowabakilia kwa kukaa katika dunia.


Kisha malaika wa saba akapiga baragumu. Halafu sauti kubwa zikasikilika katika mbingu, zikisema: “Sasa utawala juu ya dunia ni wa Bwana wetu na wa Masiya wake. Naye atatawala kwa milele na milele!”


Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mbinguni, ikisema: “Sasa wokovu, uwezo na ufalme wa Mungu, na mamlaka ya Kristo wake vimefika. Ni vile, kwa yule aliyekuwa akiwashitaki wandugu zetu mbele ya Mungu wetu muchana na usiku ametupwa chini ya mbingu.


Kisha nikasikia sauti inayosikilika kama kelele la kundi kubwa la watu, na kama ngurumo ya maporomoko ya maji mengi na kama ngurumo kubwa ya radi ikisema: “Mungu asifiwe! Kwa maana yeye Bwana wetu, Mungu wetu Mwenye Uwezo anatawala.


Kisha nikaona viti vya kifalme na watu waliokuwa wakiikaa juu yao, wakapewa uwezo wa kuhukumu. Nikaona vilevile roho za wale waliochinjwa kwa sababu ya kutangaza ukweli ulioshuhudiwa na Yesu na Neno la Mungu. Watu wale hawakumwabudu yule nyama wa ajabu, wala sanamu yake, wala hawakupigwa chapa yake juu ya paji za nyuso zao, au juu ya mikono yao. Nao wakafufuka na kutawala pamoja na Kristo muda wa miaka elfu moja.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ