Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 5:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Heri wale wanaokuwa na moyo safi, maana watamwona Mungu!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 5:8
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Yakobo akamwambia: “Tafazali, ninakuomba uniambie jina lako.” Lakini yeye akamwambia: “Kwa nini kuniuliza jina langu?” Kisha akamubariki Yakobo.


bila kosa kwa wale ambao hawafanyi makosa, lakini mukali kwa waovu.


Ni mutu anayefanya hivi: anaishi katika ukamilifu, anatenda kwa haki siku zote, anasema ukweli kutoka ndani ya moyo, hatetani, hatendei rafiki yake uovu, hamutukani jirani yake, anazarau wapotevu, anaheshimu wanaomwabudu Yawe, hageuzi kiapo chake hata kikimuletea hasara, hakopeshi feza yake kwa kupata faida, wala kupokea kituliro kumutesa asiyekuwa na kosa. Mutu anayefanya vile, hatatikisika hata kidogo.


Wewe ni mwema kwa wema, mukamilifu kwa wakamilifu,


Ni mutu wa matendo mema na moyo safi, asiyefuata mambo ya ovyo, wala kuapa kwa uongo.


Unijaze furaha na shangwe, unifurahishe tena, mimi ambaye uliniponda.


Nimekukosea wewe peke yako, nimetenda mabaya mbele yako. Hivi uamuzi wako ni wa haki, hukumu yako haipotoki.


Zaburi ya Asafu. Hakika, Mungu ni muzuri kwa Israeli, kwa watu wenye moyo safi.


Mwenye nia safi na maneno mazuri atakuwa rafiki wa mufalme.


Yeye hakufanya ubaguzi kati yetu na wao; ametakasa mioyo yao kwa sababu walimwamini.


Kwa maana wakati wa sasa tunaona kama mwenye kuangalia ndani ya kioo kisichoonyesha wazi, lakini wakati utakaokuja tutaona waziwazi. Kwa sasa ninajua tu mambo machache, lakini nyuma nitajua kwa utimilifu kama vile Mungu anavyonijua mimi.


Basi wapendwa wangu, kwa kuwa tumepewa ahadi hizi zote, tujitakase toka uchafu wote unaochafua mwili na roho na tujikaze kuwa watakatifu kabisa tukiishi katika kumuheshimu Mungu.


Kila kitu ni safi kwa watu wanaokuwa safi. Lakini hakuna chochote kinachokuwa safi kwa watu wachafu na wasiomwamini Mungu, kwa maana akili na zamiri zao zimekuwa chafu.


Basi tumwendee Mungu kwa moyo wa uaminifu, kwa imani kamilifu, kwa moyo uliosafishwa toka zamiri mbaya na mwili uliosafishwa na maji safi.


Mujikaze kwa kuishi katika amani na watu wote na kuishi katika utakatifu, kwa sababu hakuna mutu asiyeishi katika hali hiyo atakayemwona Bwana.


Ikiwa ni hivi, damu ya Kristo haitakuwa na uwezo zaidi wa kututakasa? Kwa maana kwa njia ya Roho anayeishi kwa milele, Kristo alijitoa mwenyewe kwa Mungu kuwa sadaka kamilifu. Nayo damu yake ikazitakasa zamiri zetu toka katika matendo yasiyofaa, kusudi tupate kumutumikia Mungu Mwenye Uzima.


Lakini hekima inayotoka mbinguni, kwanza ni safi, tena ni yenye amani, upole na usikilivu, inajaa huruma na matendo mema. Haina upendeleo wala udanganyifu.


Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia. Musafishe mikono yenu, ninyi wenye zambi! Mutakase mioyo yenu, ninyi wenye nia mbili!


Ninyi mumekwisha kutakaswa kwa njia ya kutii neno la kweli kwa kuwapenda wandugu zenu pasipo unafiki. Basi mupendane kabisa, kwa moyo wenu wote.


Wataona uso wake na jina lake litaandikwa juu ya paji za nyuso zao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ