Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 5:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Heri wale wanaokuwa na huruma, maana Mungu atawahurumia!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 5:7
37 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wewe ni mwema kwa wema, mukamilifu kwa wakamilifu,


Mutu wa usawa anaangaziwa mwangaza katika giza; yeye ni mwenye huruma, rehema, na haki.


Anatoa kwa moyo safi, anawapa wamasikini. Haki yake inadumu milele. Ana nguvu na sifa.


Yawe amenilipa kwa kadiri ya haki yangu; kwa kadiri ya usafi wa mikono yangu mbele yake.


Siku zote yeye anakopesha kwa moyo safi, na watoto wake ni wenye baraka.


Mutu mwema anafaidika yeye mwenyewe, lakini mutu mukali anajiumiza mwenyewe.


Mutu anayetoa kwa moyo safi atafanikishwa. Mutu anayekunywesha mwingine maji, naye atakunyweshwa.


Anayemuzarau jirani yake ni mwenye zambi, lakini ana heri yule anayekuwa mwema kwa masikini.


Anayemusaidia masikini anamukopesha Yawe; Yawe atamulipa kwa tendo lake jema.


Mutu wa haki akikufa, hakuna mutu anayejali; mutu mwema akihamishwa toka dunia, hakuna mutu anayefikiri na kusema: Mutu huyo mwema amehamishwa kusudi asipatwe na hasara,


Basi, akasema kwa sauti: Angalia Babeli, muji mukubwa nilioujenga kwa nguvu zangu ukuwe makao yangu ya kifalme na kwa ajili ya utukufu wangu!


Gomeri alipata mimba tena, akazaa mutoto mwanamuke. Yawe akamwambia Hosea: Umupange mutoto huyo jina la “Asiyehurumiwa”, maana sitawahurumia tena Waisraeli wala sitawasamehe.


Lakini hesabu ya Waisraeli itakuwa kubwa kama muchanga wa bahari ambao haupimiki wala hauhesabiki. Pale ambapo Mungu aliwaambia: Ninyi si watu wangu, sasa atawaambia: Ninyi ni watoto wa Mungu Mwenye Uzima.


Siku hiyo, nitajibu kwa mahitaji ya mbingu ya kunyesha mvua, mbingu nazo zitajibu kwa mahitaji ya udongo. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Mungu amekuonyesha yanayokuwa mema, ewe mwanadamu; kitu Yawe anachotaka kwako ni hiki: kutenda mambo ya haki, kupenda kuwa na huruma, na kuishi kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wako.


Na munaposimama kwa kuomba, mukiwa na neno na mutu mwingine, mumusamehe, kusudi Baba yenu anayekuwa mbinguni, awasamehe vilevile makosa yenu. [


Lakini muwapende waadui zenu, muwatendee mema na muwakopeshe pasipo kutumainia kurudishiwa kitu. Halafu mutapewa zawadi kubwa na mutakuwa kweli watoto wa Mungu Mukubwa kwa sababu yeye ni mwema kwa watu waovu wasiokuwa na shukrani.


Zamani ninyi mulimwasi Mungu, lakini sasa amewahurumia kutokana na uasi wa Wayuda.


Kuelekea wale ambao hawajaoa wala kuolewa, sina neno la kuwaamuru kutoka kwa Bwana. Lakini nitawatolea shauri kufuatana na vile ninavyokuwa mutu anayestahili kuaminiwa, kutokana na neema niliyopewa na Bwana.


Kwa wema wake, Mungu ametupatia utumishi huu, na kwa sababu hii sisi hatukati tumaini.


Lakini mutendeane wema ninyi kwa ninyi; musameheane kama Mungu alivyowasamehe ninyi kwa njia ya Kristo.


Ninyi ni watu wa Mungu, yeye amewapenda na kuwachagua kwa ajili yake mwenyewe. Kwa hiyo, mukuwe na moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.


Ingawa zamani nilikuwa mwenye kumutukana, mwenye kumutesa na kumutendea kwa ukali, lakini amenihurumia, kwa sababu yote niliyofanya, niliyafanya kwa upumbafu kwa maana sikukuwa bado na imani.


lakini kwa sababu hiyo Mungu amenihurumia. Alifanya vile kusudi kwa njia yangu mimi ninayekuwa mutenda zambi wa kwanza, Yesu Kristo apate kuonyesha uvumilivu wake. Na hivi mimi nipate kuwa mufano kwa wote watakaoamini nyuma na kupata uzima wa milele.


Kwa sababu hii, tujongelee kwa uhodari kiti cha kifalme cha Mungu pahali anapowajalia watu neema kusudi apate kutuhurumia na kutujalia neema ya kutusaidia kwa wakati unaofaa.


Kwa maana Mungu ni mwenye haki. Yeye hatasahau kazi yenu na upendo mulioonyesha kwa ajili yake kwa namna mulivyowasaidia watu wake na munavyoendelea kuwasaidia.


Kwa sababu Mungu hatahurumia mutu yule asiyehurumia wengine. Lakini huruma ya Mungu itaishinda hukumu.


Lakini hekima inayotoka mbinguni, kwanza ni safi, tena ni yenye amani, upole na usikilivu, inajaa huruma na matendo mema. Haina upendeleo wala udanganyifu.


Zamani ninyi hamukukuwa watu wa Mungu, lakini sasa munakuwa watu wake; zamani ninyi hamukuhurumiwa na Mungu, lakini sasa mumehurumiwa naye.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ