47 Na kama mukiwasalimia wandugu zenu tu, munatenda tendo gani la kupita wengine? Hata wapagani wanatendeana vile!
Mutakapoingia ndani ya nyumba, muwasalimie watu wanaokuwa mule, mukisema: ‘Amani kwenu.’
Basi ninawaambia: musipokuwa wenye haki kuliko walimu wa Sheria na Wafarisayo hamutapokelewa katika Ufalme wa mbinguni.
Zawadi gani mutapata kutoka kwa Mungu, kama mukiwapenda tu wenye kuwapenda? Hata walipishaji wa kodi wanaokuwa wakorofi wanatendeana vile!
Basi mukuwe wakamilifu, kama vile Baba yenu wa mbinguni anavyokuwa mukamilifu.
“Muko na shukrani gani kama munawapenda tu wale wanaowapenda? Kwa maana hata wenye zambi wanawapenda wale wanaowapenda.
Luka, muganga wetu mupendwa na Dema wanawasalimia.
Muwasalimie wandugu wa Laodikia, pamoja na Nimfa na kanisa linalokusanyika ndani ya nyumba yake.
Kuna sifa gani kama mukivumilia mapigo kwa sababu mulitenda mabaya? Lakini mukivumilia mateso kwa sababu mulitenda mema, jambo hilo linamupendeza Mungu.