Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 5:46 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

46 Zawadi gani mutapata kutoka kwa Mungu, kama mukiwapenda tu wenye kuwapenda? Hata walipishaji wa kodi wanaokuwa wakorofi wanatendeana vile!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 5:46
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mwana wa Mutu alikuja, yeye anakula na kunywa, nao wanasema: ‘Angalia huyu mulafi na mulevi, rafiki wa walipishaji wa kodi na watenda maovu wenzao.’ Lakini hekima ya Mungu ilionyeshwa kuwa ya haki kwa njia ya matendo yake.”


Na kama akikataa kuwasikia watu wale, upeleke habari kwa kanisa. Naye akikataa kusikia kanisa vilevile, umuhesabu kama mupagani na mutenda maovu sawa walipishaji wa kodi.


Na kama mukiwasalimia wandugu zenu tu, munatenda tendo gani la kupita wengine? Hata wapagani wanatendeana vile!


“Mujiangalie musifanye matendo mema mbele ya watu kusudi mujionyeshe kwao. Kwa maana mukifanya hivi hamutapata faida kutoka kwa Baba yenu anayekuwa mbinguni.


Nyuma Yesu akaikaa kula chakula ndani ya nyumba ya Lawi. Walipishaji wengi wa kodi na watenda mabaya wengine waliikaa kula pamoja na Yesu na wanafunzi wake, kwa maana watu wengi wa namna ile walikuwa wamemufuata.


Na wakati walimu wa Sheria wa kikundi cha Wafarisayo walipomwona Yesu akikula pamoja na watu wale, wakawauliza wanafunzi wake: “Kwa sababu gani anakula pamoja na walipishaji wa kodi na watenda mabaya?”


Siku moja walipishaji wa kodi na watenda mabaya wengi walikusanyika karibu na Yesu kwa kumusikiliza.


Lakini yule mulipishaji wa kodi alisimama kwa mbali, naye hakusubutu hata kuinua macho yake kuelekea mbingu; lakini alijipigapiga kwa huzuni na kusema: ‘Ee Mungu, unisamehe mimi mutenda mabaya.’ ”


Kule kulikuwa mutu mumoja jina lake Zakayo aliyekuwa mukubwa wa walipishaji wa kodi, naye alikuwa tajiri.


Watu wote walioona hayo wakaanza kunungunika wakisema: “Amekwenda kupanga kwa mutenda maovu!”


Walipishaji wa kodi nao wakamufikia vilevile kusudi wabatizwe. Wakamwuliza: “Mwalimu, tufanye nini?”


Kisha Lawi akamufanyia Yesu karamu kubwa katika nyumba yake. Walipishaji wengi wa kodi na watu wengine walikuwa wakikula pamoja nao.


Wafarisayo na walimu wa Sheria wa kikundi chao wakawanungunikia wanafunzi wake, wakisema: “Kwa sababu gani munakula na kunywa pamoja na walipishaji wa kodi na watenda mabaya?”


(Watu wote waliomusikiliza, na walipishaji wa kodi vilevile, wakakubali kwamba Mungu ni mwenye haki, hata wakabatizwa na Yoane.


Mwana wa Mutu alikuja, yeye anakula na kunywa, nanyi munasema: ‘Angalia huyu mulafi na mulevi, rafiki ya walipishaji wa kodi na watenda maovu.’


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ