Elisha akajibu: “Hapana, usiwaue. Maana hawa unaotaka kuwaua uliwateka kwa upanga wako na mushale wako? Uwape chakula na maji, wakule na kunywa kisha uwaache warudie kwa bwana wao.”
Wakati walipomutukana, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakutisha watu hata wamwogope. Lakini alijiachilia katika mikono ya Mungu anayehukumu watu kwa haki.
Musirudishiane mabaya kwa mabaya au matusi kwa matusi, lakini muombeane baraka, kwa sababu Mungu aliahidi kuwabariki ninyi wakati alipowaita kumufuata.