Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 5:44 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

44 Lakini mimi ninawaambia: muwapende waadui zenu na muwaombee wale wanaowatesa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 5:44
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Elisha akajibu: “Hapana, usiwaue. Maana hawa unaotaka kuwaua uliwateka kwa upanga wako na mushale wako? Uwape chakula na maji, wakule na kunywa kisha uwaache warudie kwa bwana wao.”


Ee Yawe, Mungu wangu! Kama nimetenda moja ya mambo haya: kama nimechafua mikono yangu kwa ubaya,


Mwenye akili hakasiriki upesi; kusamehe makosa ni utukufu kwake.


Halafu Yesu akasema: “Baba uwasamehe, kwa maana hawajui jambo wanalofanya.” Waaskari wakagawanya nguo zake kwa kuzipigia kura.


Ninawapa amri mupya: mupendane ninyi kwa ninyi. Kama mimi nilivyowapenda, nanyi mupendane vilevile.


Lakini Paulo akalalamika kwa nguvu akisema: “Usijiue, kwa maana sisi wote tuko hapa!”


Kisha akapiga magoti, akalalamika, akisema: “Bwana, usiwahesabie zambi hii.” Na nyuma ya kusema maneno haya, akakufa.


Mumwombe Mungu awabariki wale wanaowatesa; muwaombee baraka wala musiwalaani.


Muangalie vema, hata mumoja wenu asimurudishie mwenzake ubaya kwa ubaya, lakini mutafutiane wema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.


Wakati walipomutukana, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakutisha watu hata wamwogope. Lakini alijiachilia katika mikono ya Mungu anayehukumu watu kwa haki.


Musirudishiane mabaya kwa mabaya au matusi kwa matusi, lakini muombeane baraka, kwa sababu Mungu aliahidi kuwabariki ninyi wakati alipowaita kumufuata.


Daudi alipomaliza kusema, Saulo akasema: “Hiyo ni sauti yako mwana wangu Daudi?” Saulo akalia kwa sauti.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ