Lakini kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Adui yako akisikia njaa, umupe chakula; kama akisikia kiu, umupe kinywaji. Maana kwa kufanya hivi utamupatisha haya kama vile ungemubebesha makaa ya moto juu ya kichwa.”
Kwa maana Mungu ni mwenye haki. Yeye hatasahau kazi yenu na upendo mulioonyesha kwa ajili yake kwa namna mulivyowasaidia watu wake na munavyoendelea kuwasaidia.
Dini inayokuwa safi na bila kosa mbele ya Mungu Baba ndiyo hii: kushugulikia wayatima na wajane wanaoteswa, na kujilinda mwenyewe na uchafu wa dunia hii.