Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 5:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

30 Na kama mukono wako wa kuume ukikukosesha, uukate na kuutupa mbali. Ni heri kwako kupoteza kiungo chako kimoja kuliko mwili wako wote muzima kutupwa katika jehenamu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 5:30
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Heri mutu yule mimi sitakayekuwa kikwazo kwake!”


Lakini halizami ndani yao kama mizizi. Wanalishika kwa muda mufupi tu. Wakati taabu na mateso vinapowafikia kwa ajili ya Neno la Mungu, mara moja, wanaanguka.


Lakini Yesu akageuka na kumwambia: “Ondoka hapa karibu nami, wewe Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu, kwa maana mawazo yako si ya Mungu, lakini ni ya kimutu.”


Lakini haifai kuwakwaza. Kwa hiyo kwenda kwenye ziwa, na utupe ndoana ndani ya maji. Na samaki wa kwanza utakayemunasa, ufungue kinywa chake, nawe utaona kikoroti cha feza. Ukikamate na kukitoa kwa kulipa kodi kwa ajili yetu sisi wawili.”


“Kama mukono wako au muguu wako ukikukosesha, uukate na kuutupa mbali! Ni heri kwako kuingia kwenye uzima wa kweli ukikuwa na mukono mumoja au ukikuwa kilema. Hiyo ni vizuri kuliko kuwa na mikono miwili au miguu miwili na kutupwa katika moto kwa milele.


Halafu mufalme akawaambia watumishi wake: ‘Mumufunge mutu huyu miguu na mikono na kumutupa inje kwenye giza. Kule atalia na kusaga meno.’ ”


Yule mutumishi aliyepewa furushi tano za zahabu, akakuja, akaleta faida ya zingine tano. Na akasema: ‘Bwana, umenipatia furushi tano za zahabu, na sasa angalia, kuna faida ya zingine tano.’


Halafu Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Usiku huu ninyi wote mutaanguka kwa ajili yangu, kwa maana imeandikwa hivi katika Maandiko Matakatifu: ‘Nitamwua muchungaji, na kondoo wa kundi watasambazwa.’


Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayemukasirikia ndugu yake anapaswa kuhukumiwa. Naye anayemwambia ndugu yake: ‘Hauna akili wewe!’ anapaswa kupelekwa kwenye tribinali kubwa. Naye anayemwambia: ‘Uko mwenda-wazimu!’ anastahili kutupwa katika jehenamu.


Basi kama jicho lako la kuume likikukosesha, uliongoe na kulitupa mbali. Ni heri kwako kupoteza kiungo chako kimoja kuliko mwili wako wote muzima kutupwa katika jehenamu.


Kama mukono wako ukikukosesha, uukate! Ni heri kwako kuingia kwenye uzima wa kweli ukiwa na mukono mumoja, kuliko kuwa na mikono miwili na kwenda katika jehenamu ndani ya moto usiozimika. [


Nitawaonyesha yule munayepaswa kumwogopa; mumwogope Mungu, kwa sababu kisha kuuawa ni yeye anayekuwa na uwezo wa kumutupa mutu katika jehenamu. Hakika ninawaambia, ni huyo munayepaswa kumwogopa!


Ingekuwa heri afungiwe jiwe kubwa la kusagia katika shingo na kutumbukizwa ndani ya bahari, kuliko kumwangusha mumoja wa wadogo hawa.


kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Angalia, ninaweka jiwe la kukwalisha katika Sayuni nalo ni la kuangusha. Lakini yule anayemwamini hatapata haya.”


Kwa hiyo chakula kikimwangusha ndugu yangu katika zambi, nitajizuiza kula nyama siku zote kusudi nisimwangushe ndugu yangu.


Wandugu, ikiwa mimi ningali ninahubiri ya kama ni lazima kutahiriwa, basi kwa sababu gani ningali ninateswa? Kama ningefanya vile, basi watu hawangechukizwa na mahubiri yangu juu ya musalaba wa Kristo.


Tena imeandikwa kwamba: “Jiwe lile ni la kukwalisha watu, nalo ni la kuwaangusha.” Wamejikwaa kwa sababu hawakuamini neno la Mungu, na hivi ndivyo walivyopanga kwa ajili yao tangu mwanzo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ