Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 5:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Basi kama ukienda kumutolea Mungu sadaka juu ya mazabahu na pale ukikumbuka kwamba ndugu yako yuko na neno juu yako,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 5:23
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu, yule mutunza vinywaji mukubwa akamwambia mufalme: “Leo ninakumbuka makosa yangu!


Mufalme aliendelea kumwambia Simei: “Unayajua wazi maovu uliyomutendea baba yangu Daudi. Sasa, kwa sababu ya hayo, Yawe atakuazibu.


Ninafikiri juu ya hayo siku zote, nayo roho yangu imejaa huzuni.


Nitakusamehe kila kitu ulichotenda. Nawe utakapokumbuka hayo yote uliyotenda utashangaa na kunyamaza kwa sababu ya haya wala hautasubutu kusema tena. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Maana kitu ninachotaka kwenu ni wema na si sadaka, kumujua Mungu na si kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto.


Ninyi vipofu! Ni nini inayokuwa kubwa zaidi, sadaka au mazabahu ndiyo inayoifanya sadaka ile ihesabiwe kuwa takatifu?


uache sadaka yako pale mbele ya mazabahu na uende kwanza kusikilizana naye. Na kisha urudie na kutoa sadaka yako.


Kisha Yesu akamwambia: “Angalisho, usimwambie mutu neno juu ya hii. Lakini kwenda na kumwonyesha kuhani jinsi unavyokuwa sasa. Kisha utoe sadaka kama Musa alivyoamuru, kuwa ushuhuda kwa watu wote kwamba umetakaswa.”


Na munaposimama kwa kuomba, mukiwa na neno na mutu mwingine, mumusamehe, kusudi Baba yenu anayekuwa mbinguni, awasamehe vilevile makosa yenu. [


Lakini Zakayo akasimama mbele ya Bwana na kumwambia: “Bwana! Ninawapa masikini nusu ya mali zangu, na kama nimetwaa kitu cha mutu kwa kumudanganya, nitamurudishia mara ine sawa na kitu kile.”


Halafu Samweli akamwambia: “Unazani kwamba Yawe anapendelea zaidi sadaka za kuteketezwa kwa moto na matoleo mengine, kuliko kuitii sauti yake? Hapana. Kumutii yeye ni bora kuliko matoleo na kumusikiliza kuliko kumutolea mafuta ya beberu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ