Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 5:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayemukasirikia ndugu yake anapaswa kuhukumiwa. Naye anayemwambia ndugu yake: ‘Hauna akili wewe!’ anapaswa kupelekwa kwenye tribinali kubwa. Naye anayemwambia: ‘Uko mwenda-wazimu!’ anastahili kutupwa katika jehenamu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 5:22
93 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini wandugu zake walipoona kwamba baba yao alimupenda Yosefu kuliko wao, wakamuchukia hata hawakuzungumuza naye kwa amani.


Wandugu zake wakamwuliza: “Unataka kutuambia kwamba utatutawala? Au utakuwa na mamlaka juu yetu?” Basi, wakazidi kumuchukia kwa sababu ya ndoto na maneno yake.


Simei alimulaani Daudi akisema: “Kwenda! Kwenda, wewe mwuaji, mutu wa ovyoovyo!


Daudi aliporudi kwake kwa kuibariki jamaa yake, Mikali, binti ya Saulo, alikwenda kumupokea, akasema: “Ni ajabu kwa mufalme wa Waisraeli kujiheshimu leo, kwa kujifunua uchi wake mbele ya watumishi wake na wajakazi wake sawa vile mushenzi anavyovua nguo zake mbele ya watu bila haya!”


Hapo, Ahabu akarudi kwake akijaa chuki na huzuni nyingi, kwa sababu Naboti wa Yezereheli alimwambia kwamba hatamupa kile alichorizi kutoka kwa wazee wake. Basi, akalala kwenye kitanda, akaficha uso wake na kukataa chakula.


Kwa hiyo, Asa akamukasirikia sana nabii Hanani, hata akamuweka katika kifungo; maana amekuwa na hasira kubwa naye juu ya maneno yale. Wakati uleule, Asa akaanza kuwatesa vikali wamoja kati ya watu.


Akaweka waamuzi katika miji yote ya Yuda yenye kuta,


Nikasema: “Kulingana na uwezo tunaokuwa nao, tumekuwa tukiwanunua tena wandugu zetu Wayuda waliokuwa wameuzishwa kwa watu wa mataifa mengine. Lakini sasa hata munawauzisha wandugu zenu, nasi tunalazimika kuwanunua!” Basi wakanyamaza kimya, bila kuwa na la kujibu.


Wanasema maovu juu yangu, na kunishambulia bila sababu.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi. Mupumbafu anajisemesha hivi katika moyo: “Hakuna Mungu.” Wote wamepotoka kabisa, matendo yao ni ya kuchukiza; hakuna hata mumoja anayetenda mazuri!


Usimwache anayekutumainia kupata haya; lakini wafezeheke wote wanaokuasi kwa makusudi.


Usiwaache waadui hao wabaya wanisimange, hao wanaonichukia bure, wafurahie mateso yangu.


Usiwake hasira wala kuwa na kasirani; usihangaike, maana hiyo inazidisha ubaya.


kimwezeshe aendelee kuishi siku zote, bila kuona kaburi.


Ninaregea kwa ajili ya kulalamika, na koo langu limekauka. Macho yangu yamefifia, nikikungojea ewe Mungu wangu.


Ee Yawe, Mungu wangu! Kama nimetenda moja ya mambo haya: kama nimechafua mikono yangu kwa ubaya,


Matendo yako, ee Yawe, ni makubwa sana! Mawazo yako hayatambulikani!


Mwenye hekima ni mwangalifu na anaepuka uovu, lakini mupumbafu hajizuizi wala hana uangalifu.


Maneno ya mupumbafu yanaleta ugomvi; kila neno analosema linasababisha azabu.


Mutu anayepata mali isiyokuwa ya usawa ni kama kwale anayelalia mayai ambayo hakutaga. Mali yanamwishia angali kijana, na kwa mwisho anageuka sawa mupumbafu.


Nimewindwa kama ndege na hao wanaonichukia bila sababu.


Halafu mufalme Nebukadneza, akakasirika, akaamuru Sadiraki, Mesaki na Abedenego waletwe mbele yake. Nao wakawaleta mbele ya mufalme.


Kwa hiyo, mufalme Nebukadneza akawaka hasira, sura yake ikabadilika kwa chuki juu ya Sadiraki, Mesaki na Abedenego. Akaamuru kwamba moto wa furu uongezwe mara saba kuliko kawaida yake.


Kwa sababu ya mateso makali muliyowatendea wandugu zenu wazao wa Yakobo, mutafezeheshwa na kuangamizwa milele.


Hamukupaswa kuangalia tu siku hiyo wandugu zenu walipopatwa na taabu, hamukupaswa kufurahi juu ya Wayuda siku hiyo walipoangamizwa, hamukupaswa kujivuna siku ile wenzenu walipokuwa wanateseka,


Mujilinde, kwa maana watu watawapeleka mbele ya tribinali kubwa nao watawapiga fimbo ndani ya nyumba zao za kuabudia.


Musiwaogope wale wanaoweza kuua tu mwili, lakini wasioweza kuua roho. Lakini zaidi mumwogope Mungu anayeweza kuharibu mwili pamoja na roho katika jehenamu.


Lakini wakati Wafarisayo waliposikia maneno yale, wakasema: “Ni Belzebuli, mukubwa wa pepo ndiye anayemupa mutu huyu uwezo wa kufukuza pepo.”


Naye alipokuwa angali akisema, wingu lenye kuangaza likawafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana. Mumusikilize!”


Kisha Petro akamwendea Yesu na kumwuliza: “Bwana, ndugu yangu akiendelea kunikosea, nitamusamehe mpaka mara ngapi? Mara saba inatosha?”


Yesu akaongeza kusema: “Ni hivi vilevile Baba yangu anayekuwa mbinguni atakavyowatendea ninyi, kama kila mumoja wenu asipomusamehe ndugu yake kwa moyo wake wote.”


“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munasafiri kuvuka bahari na inchi mbalimbali kusudi mupate kumugeuza hata mutu mumoja tu kuwa mufuasi wenu. Nanyi munapomupata, munamufanya kuwa mwenye kustahili azabu ya jehenamu mara mbili zaidi kuliko ninyi.


Ninyi kikundi cha nyoka! Namna gani mutaweza kuepuka azabu ya jehenamu?


“Kisha mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kushoto: ‘Muondoke hapa karibu nami, ninyi muliolaaniwa! Muende katika moto usiozimika hata milele, uliotayarishwa kwa ajili ya Shetani na wamalaika wake!


Wakubwa wa makuhani na wakubwa wote wa Baraza Kubwa walitafuta mashitaki ya uongo juu ya Yesu, kusudi wapate kumwua.


Na sauti ikasikilika toka mbinguni, ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa naye sana.”


Lakini mimi ninawaambia: musiape hata kidogo kwa jina la mbingu, kwa maana ni kiti cha kifalme cha Mungu;


Lakini mimi ninawaambia: muwapende waadui zenu na muwaombee wale wanaowatesa.


Wakubwa wa makuhani na wakubwa wote wa Baraza Kubwa walitafuta mashitaki juu ya Yesu kusudi wapate kumwua, lakini hawakupata neno.


Asubui mapema, mara moja wakubwa wa makuhani wakafanya shauri pamoja na wasimamizi wa watu, walimu wa Sheria na wakubwa wote wa baraza. Wakamufunga Yesu, wakamupeleka na kwenda kumutoa kwa Pilato.


Nitawaonyesha yule munayepaswa kumwogopa; mumwogope Mungu, kwa sababu kisha kuuawa ni yeye anayekuwa na uwezo wa kumutupa mutu katika jehenamu. Hakika ninawaambia, ni huyo munayepaswa kumwogopa!


Usiku ulipokucha, wazee wa Wayuda, wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria, wakakusanyika. Wakamuleta Yesu mbele ya Baraza yao Kubwa,


Basi wakubwa wa makuhani na Wafarisayo wakakusanya Baraza yao Kubwa, na kusema: “Tufanye nini kwa kuona mutu huyu anaonyesha vitambulisho vingi?


Lakini wamefanya hivi kusudi maneno haya yaliyoandikwa katika Sheria yao yatimie: ‘Wamenichukia pasipo sababu.’


Watu wale wakajibu: “Wewe uko na pepo. Nani anatafuta kukuua?”


Wayuda wakamujibu: “Sisi tulikuwa na haki ya kusema kwamba wewe ni Musamaria na kwamba uko na pepo.”


Walimu wamoja wa kikundi cha Waepikurio na cha Wastoiko, wakaanza kubishana na Paulo. Wamoja wao wakauliza: “Huyu katetea anataka kusema nini?” Wengine wakasema: “Anaonekana kuwa muhubiri wa miungu ya kigeni.” Walisema hivi kwa sababu Paulo alikuwa akihubiri juu ya Yesu na jinsi alivyofufuka.


Kesho yake, jemadari alitaka kujua mashitaki kamili ya Wayuda juu ya Paulo. Kwa hiyo akamufungua na kuamuru wakubwa wa makuhani pamoja na Baraza Kubwa wafanye mukutano. Kisha akamuleta Paulo na kumusimamisha mbele yao.


Paulo akawakazia macho wale washauri wa Baraza Kubwa na kusema: “Wandugu zangu, mpaka leo zamiri yangu hainihukumu juu ya kitu chochote kinachoelekea mwenendo wangu mbele ya Mungu.”


Au watu hawa wanaokuwa hapa waseme kosa waliloniona nalo wakati niliposambishwa mbele ya Baraza Kubwa.


Basi wakawaamuru watoke katika Baraza Kubwa na kwenda inje, nao wakaulizana shauri wao kwa wao,


Na sawa vile walivyoambiwa, asubui mapema wakaingia ndani ya hekalu, na kuanza kuwafundisha watu. Kuhani Mukubwa na wale washiriki walipofika, wakawakusanya wasimamizi wote wa Waisraeli kwa kufanya mukutano wa Baraza Kubwa. Nao wakawatuma watu kwenye kifungo kwa kuwaleta mitume.


Walipokwisha kuwaleta, wakawasimamisha mbele ya Baraza Kubwa. Naye Kuhani Mukubwa akaanza kuwasambisha,


Basi wakawachochea watu, wazee, na walimu wa Sheria. Nao wakamufikia Stefano, wakamukamata na kumupeleka mbele ya Baraza Kubwa.


Na wote waliohuzuria katika lile Baraza wakamukazia Stefano macho, wakaona uso wake unafanana sawa na uso wa malaika.


Ni yule yule Musa ndiye aliyewaambia watu wa Israeli: ‘Mungu atawatumia ninyi nabii anayekuwa sawa mimi, toka katika taifa lenu.’


Mupendane ninyi kwa ninyi kwa kweli kama vile wandugu, nanyi muheshimiane ninyi kwa ninyi.


wizi, wenye tamaa, walevi, watukanaji, wanyanganyi, watu wale wote hawatapata urizi katika Ufalme wa Mungu.


Lakini sasa ndugu mwamini anamushitaki mwenzake mbele ya waamuzi wasioamini.


Wamasikini hawatakosekana katika inchi; hivyo ninawaamuru, mukuwe wenye moyo safi kwa wandugu zenu wenye mahitaji na wamasikini katika inchi yenu.


“Mutachagua waamuzi na wakubwa kutoka makabila yenu katika miji yenu ambayo Yawe, Mungu wenu, atawapa nao watatoa hukumu za haki kwa watu.


Kuelekea maneno hayo, mutu yeyote asimukosee ndugu yake wala kumudanganya. Tumekwisha kuwaambia na kuwahakikishia mbele kwamba Bwana atawaazibu wale wanaofanya mambo kama hayo.


Uwaambie wasiseme mabaya juu ya mutu, lakini wakuwe wenye kupenda amani na wema, na wenye kuonyesha upole mbele ya kila mutu.


Basi muangalie vizuri kusudi musikatae kumusikiliza yule anayesema nanyi. Wale waliokataa kusikiliza yule aliyewaonya hapa katika dunia hawakuponyoka azabu ya Mungu. Si jambo hilo linaonyesha wazi kwamba sisi hatutaweza kuponyoka kama tunamugeuzia mugongo yule anayetutolea maonyo kutoka mbinguni?


Na alipokwisha kufanywa kuwa mukamilifu, akawaongoza watu wote wanaomutii wapate kuokolewa kwa milele.


Wewe mujinga! Unataka kuhakikishwa kwamba imani pasipo matendo ni bure?


Nao ulimi ni kama moto. Ulimi ni kiungo kinachojaa ubaya wa kila namna. Ulimi unapatikana kwenye nafasi yake katikati ya viungo vyetu, nao ndio unaochafua mwili wote. Unateketeza maisha yetu ukichomwa wenyewe na moto unaotoka katika jehenamu.


Wakati walipomutukana, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakutisha watu hata wamwogope. Lakini alijiachilia katika mikono ya Mungu anayehukumu watu kwa haki.


Musirudishiane mabaya kwa mabaya au matusi kwa matusi, lakini muombeane baraka, kwa sababu Mungu aliahidi kuwabariki ninyi wakati alipowaita kumufuata.


Mutu anayesema kwamba anaishi katika mwangaza, lakini anamuchukia ndugu yake, yeye angali anaishi katika giza.


Hii ndiyo njia inayoonyesha wazi tofauti kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Shetani. Mutu asiyetenda mambo ya haki au asiyemupenda ndugu yake si mutoto wa Mungu.


Mutu akimwona ndugu yake anafanya zambi isiyoleta kifo, anapaswa kumwombea kwa Mungu, Mungu atamupa mutu yule uzima. Jambo hili linaelekea wale wanaotenda zambi isiyoleta kifo. Maana kuna zambi inayoleta kifo lakini sisemi kama ataomba juu ya hiyo.


Hata Mikaeli, malaika mukubwa, aliposhindana na kubishana na Shetani juu ya maiti ya Musa, hakusubutu kumuhukumu kwa matusi, lakini alisema: “Bwana mwenyewe akukaripie.”


Kisha kifo na kuzimu vikatupwa katika ziwa la moto. Ziwa lile la moto ndicho kifo cha pili.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ