Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 5:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Basi ninawaambia: musipokuwa wenye haki kuliko walimu wa Sheria na Wafarisayo hamutapokelewa katika Ufalme wa mbinguni.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 5:20
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu wanafunzi wakafahamu kwamba Yesu hakuwaambia kwamba wafanye angalisho na chachu ya mikate, lakini na mafundisho ya Wafarisayo na Wasadukayo.


Naye anayemupokea mutoto mudogo kama huyu kwa ajili ya jina langu, ananipokea mimi.


Shoka limekwisha kuwekwa tayari kwenye mashina ya miti. Kila muti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa katika moto.


“Si kila mutu anayeniita ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa mbinguni, lakini yule tu anayefanya mapenzi ya Baba yangu anayekuwa mbinguni.


Kweli ninawaambia ninyi: mutu yeyote asiyepokea Ufalme wa Mungu kama mutoto mudogo, hawezi kuingia ndani yake hata kidogo.”


Ni kwepesi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu.”


Ole kwenu! Munafanana na makaburi yasiyoonekana wazi ambayo watu wanatembea juu yao pasipo kujua.”


Wakati ule ule makundi mengi ya maelfu ya watu walikusanyika hata wakakanyaganakanyagana. Yesu akaanza kwanza kusema na wanafunzi wake, akiwaambia: “Mufanye angalisho na chachu ya Wafarisayo, maana yake unafiki wao.


Kweli ninawaambia: ‘Mutu yeyote asiyekubali Ufalme wa Mungu kama mutoto mudogo, hawezi kuingia katika Ufalme ule hata kidogo.’ ”


Ikiwa utumishi unaowaletea watu hukumu ulikuwa na utukufu, basi si zaidi sana utumishi unaowafanya watu wahesabiwe haki mbele ya Mungu, utakuwa na utukufu mukubwa zaidi?


Basi mutu yeyote anapoungana na Kristo, yeye anakuwa kiumbe kipya. Mambo ya zamani yametoweka, na sasa hali mupya imefika.


na kuungana naye kabisa. Nami sihesabiwi haki tena kufuatana na mambo niliyofanya, ndiyo ile haki inayopatikana kwa njia ya kushika Sheria. Lakini ninahesabiwa haki kwa njia ya kumwamini Kristo, ndiyo ile haki inatoka kwa Mungu, naye anamuhesabia haki yule anayeamini.


Mujikaze kwa kuishi katika amani na watu wote na kuishi katika utakatifu, kwa sababu hakuna mutu asiyeishi katika hali hiyo atakayemwona Bwana.


Hakuna kitu chochote kichafu kitakachoingia ndani yake, wala yeye anayefanya machukizo na kusema uongo; lakini wale tu ambao majina yao yaliandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ