Akaniuliza: Unaona nini? Nami nikamujibu: Ninaona kinara cha taa cha zahabu. Juu yake kuna bakuli la mafuta na taa saba, na kila moja ina pahali pa kutilia tambi saba.
Basi kama mwili wako wote uko katika mwangaza pasipo kiungo kinachokuwa katika giza, mwili wako wote utabaki katika mwangaza kabisa, kama vile taa inavyokuangazia kwa mwangaza wake.”
“Hakuna mutu anayewakisha taa na kuifunika na chombo fulani au kuiweka chini ya kitanda. Lakini anaiweka juu ya kinara kusudi wanaoingia ndani wapate kuona mwangaza.
kusudi mupate kuwa bila kosa na kuwa na maisha safi. Hivi mutakuwa watoto wakamilifu wa Mungu wasiokuwa na kilema kati ya watu waovu na wapotovu wa dunia hii. Munapaswa kuangaza kati ya watu hawa kama vile nyota zinavyoangaza katika mbingu,
Kufuatana na ile, kulikuwa Hema iliyosimikwa. Chumba chake cha kwanza kiliitwa Pahali Patakatifu. Ndani ya chumba kile kulikuwa kinara cha kuwekea taa, meza na mikate iliyotolewa kwa Mungu.