Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 5:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 “Ninyi ni kama mwangaza katika dunia. Muji unaojengwa juu ya mulima hauwezi kufichama.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 5:14
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Njia ya wenye haki ni kama mwangaza wa asubui mapema, ambao unaangaza zaidi na zaidi hata muchana kamili.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ndivyo itakavyokuwa juu ya Yerusalema. Mimi niliuweka kuwa katikati ya mataifa, umezungukwa na inchi za kigeni pande zote.


Basi muaminie mwangaza ule wakati mungali nao, kusudi mukuwe watu wa mwangaza.” Yesu alipokwisha kusema maneno hayo, akajiendea na kujificha mbali na lile kundi.


Yoane alikuwa kama taa inayowaka na kuangaza, na ninyi mulipendezwa kufurahishwa na mwangaza wake kwa muda.


Yesu akawaambia watu tena: “Mimi ni mwangaza wa dunia. Yeye anayenifuata hatatembea katika giza hata kidogo, lakini atakuwa na mwangaza wa uzima.”


Wakati nikingali katika dunia, mimi ni mwangaza wa dunia.”


Musishirikiane pamoja na watu wasioamini. Kwa maana kuna ushirika gani kati ya haki na uovu? Kuna mapatano gani kati ya mwangaza na giza?


kusudi mupate kuwa bila kosa na kuwa na maisha safi. Hivi mutakuwa watoto wakamilifu wa Mungu wasiokuwa na kilema kati ya watu waovu na wapotovu wa dunia hii. Munapaswa kuangaza kati ya watu hawa kama vile nyota zinavyoangaza katika mbingu,


Kwa maana ninyi wote ni watu wanaoishi katika mwangaza, ndio watu wa muchana. Sisi si watu wa usiku wala wa giza.


Hii ndiyo maana ya lile fumbo juu ya zile nyota saba ulizoona katika mukono wangu wa kuume, na vile vinara saba vya zahabu: zile nyota saba ni wamalaika wa makanisa saba na vile vinara saba ni yale makanisa saba.


Basi kumbuka jinsi ulivyokuwa ulipokuwa haujaanguka, ugeuke toka zambi zako na kurudilia yale matendo yako ya kwanza. Kama usipogeuka toka zambi zako, nitakuja kwako na kuongoa kinara chako toka pahali pake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ