Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 5:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Mufurahi na kushangilia, kwa sababu munawekewa zawadi kubwa mbinguni. Ni hivi walivyowatesa manabii walioishi mbele yenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 5:12
51 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nyuma ya mambo hayo, neno la Yawe lilimufikia Abramu katika maono kusema hivi: “Abramu! Usiogope! Mimi ni ngao yako. Zawadi yako itakuwa kubwa!”


Hauna habari kwamba Yezebeli alipokuwa akiwaua manabii wa Yawe, mimi niliwatwaa manabii mia moja nikawaficha makumi tano tano katika pango, nikakuwa ninawapatia chakula na maji?


na wakati Yezebeli alipowaua manabii wa Yawe, Obadia aliwachukua manabii mia moja, akawaficha makumi tano tano ndani ya pango, akakuwa anawapelekea chakula na maji.


Yezebeli akatuma mujumbe kwa Elia amwambie: “Miungu waniue, ninakuapia, kama kesho nisipokuua kwa wakati kama huu sawa vile ulivyowaua wale manabii.”


Basi, Ahabu alipomwona Elia, akasema: “Ewe adui yangu, umeninasa tena?” Elia akamujibu: “Ndiyo! Nimekunasa, kwa sababu wewe umekusudia kabisa kutenda maovu mbele ya Yawe.


Naye mufalme wa Israeli akamujibu Yosafati: “Kungali mumoja, Mikaya mwana wa Imula. Yeye tunaweza kumwomba shauri la Yawe. Lakini ninamuchukia sana kwa sababu yeye, hatabiri jambo zuri juu yangu hata kidogo, lakini baya tu.” Yosafati akamwambia: “Si vizuri kwa mufalme kusema hivyo.”


Halafu akamutuma kiongozi mumoja wa waaskari na watu wake makumi tano wamulete Elia. Kiongozi huyo akaenda, akamukuta Elia akiikaa kwenye mulima, akamwambia: “Ewe mutu wa Mungu, mufalme anakuamuru ushuke.”


Kwa hiyo, Asa akamukasirikia sana nabii Hanani, hata akamuweka katika kifungo; maana amekuwa na hasira kubwa naye juu ya maneno yale. Wakati uleule, Asa akaanza kuwatesa vikali wamoja kati ya watu.


Lakini wao waliendelea kuwachekelea wajumbe wa Mungu, wakayazarau maneno yake na kuwachekelea manabii wake mpaka kwa mwisho kasirani ya Yawe ikawaka juu ya watu wake hata hakukukuwa wa kuwaponyesha.


Lakini hawakukuwa waaminifu kwako. Wakakuasi, wakaacha sheria yako na kuwaua manabii waliowaonya kusudi wakurudilie wewe. Wakatenda zambi kubwa mbele yako.


Yanatamanika kuliko zahabu, kuliko zahabu safi kabisa. Ni matamu kuliko asali, kuliko asali safi kabisa.


Watu wa haki watafurahi wanapoona waovu wanaazibiwa; watatembea katika damu ya watu wabaya.


Faida mwovu anayopata ni ya uongo, lakini anayetenda mema, hakika atapata faida.


Muwaambie watu wa haki jinsi wanavyokuwa na heri, maana watakula matunda ya matendo yao.


Niliwaazibu ninyi lakini ilikuwa bure, ninyi munakataa maonyo. Muliwateketeza manabii wenu kwa upanga kama simba mwenye uchu.


Basi Yeremia alipomaliza kutangaza mambo yote ambayo Yawe aliyomwamuru kutangaza kwa watu wote, makuhani, manabii na watu wote walimukamata na kusema: Wewe unapaswa kuuawa!


Yeremia akamwambia: Huo ni uongo! Mimi sitoroki na kwenda kujiunga na Wakaldea. Lakini Iria hakusadiki maneno ya Yeremia. Basi akamutia katika kifungo na kumupeleka kwa wakubwa.


Kwa maana Mwana wa Mutu atakuja na wamalaika akitukuzwa na Baba yake, halafu atamulipa kila mutu kufuatana na matendo yake.


“Munapofunga kula chakula, musifanye kama wanafiki, wanaojigeuza kuwa wenye sikitiko na kukunja nyuso zao, kusudi watu waone kwamba wanafunga. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.


“Ewe Yerusalema, Ewe Yerusalema, wewe unayewaua manabii na wajumbe ambao Mungu anakutumia kwa kuwatupia mawe. Mara nyingi nilitaka kuwakusanya wakaaji wako kama vile kuku anavyokusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake, lakini ninyi hamukutaka!


Mambo hayo yatakapotokea, mufurahi na kurukaruka, maana munawekewa zawadi kubwa mbinguni. Ni hivi babu zao walivyowatendea manabii.


Lakini muwapende waadui zenu, muwatendee mema na muwakopeshe pasipo kutumainia kurudishiwa kitu. Halafu mutapewa zawadi kubwa na mutakuwa kweli watoto wa Mungu Mukubwa kwa sababu yeye ni mwema kwa watu waovu wasiokuwa na shukrani.


Na katikati ya usiku, Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za sifa, nao wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza.


Basi mitume wakatoka katika baraza, wakifurahi sana kwa sababu walistahili kuzarauliwa kwa kuteswa kwa ajili ya Yesu.


Zaidi ya hii, tunafurahi vilevile kwa ajili ya mateso tunayopata, kwa sababu tunajua kwamba mateso yanaleta uvumilivu,


Yule anayepanda na yule anayenyweshea maji wote ni sawa; naye Mungu atamupa kila mutu mushahara wake kufuatana na kazi aliyofanya.


Kwa maana taabu tunayopata ni ndogo na ya muda tu, inatutayarishia utukufu mukubwa sana na wa milele unaokuwa muzuri zaidi kupita mateso haya.


Kwa maana Mungu amewapa ninyi neema ya kumutumikia Kristo, na si kwa kumwamini tu, lakini vilevile kwa kuteswa kwa ajili yake.


Hata nikitoa maisha yangu kuwa sadaka pamoja na imani yenu inayokuwa sadaka mbele ya Mungu, mimi ninafurahi na kushiriki pamoja nanyi wote.


Sasa ninafurahi kwa ajili ya mateso ninayopata juu yenu. Kwa njia ya kuteseka kwangu kimwili, ninatimiza mateso yaliyomubakilia Kristo kwa ajili ya mwili wake, maana yake kanisa.


Mukumbuke kwamba Bwana atawapa ninyi zawadi ile anayowawekea watu wake. Kwa maana Kristo ndiye Bwana wa kweli munayemutumikia.


Ndio wale waliomwua Bwana Yesu na manabii, wakatutesa sisi vilevile. Wao hawamupendezi Mungu, nao ni waadui za watu wote!


Muliwahurumia wale waliokuwa katika kifungo, nanyi mulikubali kwa furaha kunyanganywa mali zenu, kwa sababu mulijua kwamba muko na mali inayokuwa bora zaidi na yenye kudumu.


Aliona kwamba kupatishwa haya kwa ajili ya Kristo kuna faida kubwa zaidi kuliko kupata utajiri wote wa inchi ya Misri, maana alikuwa anatazamia kupokea zawadi yake.


Kwa njia ya imani hawa walishinda inchi za wafalme, walitenda mambo ya haki na kupata yale Mungu aliyowaahidi. Walifunga vinywa vya simba,


Basi pasipo imani, hakuna mutu anayeweza kumupendeza Mungu. Kwa maana mutu anayetaka kumwendea Mungu sherti aamini kwamba Mungu yuko, na kwamba anawapa zawadi wale wanaomutafuta.


Wandugu zangu, muhesabu kuwa ni jambo la furaha sana wakati munapopata majaribu ya namna mbalimbali,


Wandugu zangu, mukumbuke manabii waliotabiri kwa jina la Bwana, muangalie namna walivyovumilia katika mateso, nanyi mufuate mufano wao.


Lakini mufurahi kwa sababu munashiriki katika mateso ya Kristo. Na kwa hiyo mutashangilia kwa furaha wakati atakapoonekana katika utukufu.


Yawe akubariki kwa yote uliyoyafanya. Yawe wa Israeli uliyemukimbilia akulinde chini ya mabawa yake, akupe zawadi kamilifu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ