Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 4:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Halafu Shetani akamupeleka katika Yerusalema, muji mutakatifu, akamusimamisha kwenye pembe la juu sana la hekalu, na kumwambia:

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 4:5
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Chumba cha sehemu ya kuingilia kilikuwa na urefu wa metre kenda, sawa na upana wa nyumba hiyo, na urefu kwenda juu metre makumi tano na ine. Kuta zake zilifunikwa kwa zahabu safi upande wa ndani.


Kisha, viongozi wa watu wakakaa katika Yerusalema; watu wengine wote, wakapiga kura kati ya kila jamaa kumi kwa kuchagua jamaa moja itakayokaa katika Yerusalema, muji mutakatifu. Jamaa zingine tisa zikakaa katika miji yao mingine.


Walawi wote waliokaa katika Yerusalema, muji mutakatifu, walikuwa mia mbili makumi munane na wane.


Ninyi munaona utukufu kujiita watu wa muji mutakatifu, na kujidai kumutegemea Mungu wa Israeli, ambaye jina lake ni Yawe wa majeshi.


Amuka! Amuka! Ujipatie zile nguvu zako, ewe Sayuni! Uvae nguo yako nzuri, ewe Yerusalema, muji mutakatifu. Maana hawataingia tena kwako watu wasiotahiriwa na wachafu.


Ee Bwana, kwa kadiri ya matendo yako ya haki usiukasirikie wala kuwa na hasira kwa ajili ya muji wako Yerusalema, mulima wako mutakatifu. Watu wote wa inchi za jirani wanauzarau Yerusalema na watu wako, kwa sababu ya zambi zetu na maovu babu zetu waliyotenda.


Muda wa miaka saba mara makumi saba umewekwa kwa ajili ya watu wako na juu ya muji wako mutakatifu kwa kumaliza makosa, kukomesha zambi, kusamehe uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri juu ya maono na unabii na kupakaa mafuta katika Pahali Patakatifu Sana.


Wakatoka ndani ya makaburi, na nyuma ya kufufuka kwa Yesu, wakaingia katika muji mutakatifu Yerusalema, na watu wengi wakawaona.


Halafu Shetani akamupeleka Yerusalema. Akamusimamisha juu sana kwenye pembe la hekalu na kumwambia: “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, ujitupe chini,


Yesu akamujibu: “Wewe hauna mamlaka yoyote juu yangu, isipokuwa tu yale uliyopewa na Mungu toka juu. Ni kwa hiyo, yule aliyenitoa kwako anabeba zambi kubwa zaidi.”


Lakini uache kiwanja kinachokuwa inje ya hekalu, usikipime kwa maana kimetolewa kwa watu wa mataifa mengine watakaokanyaga muji mutakatifu kwa muda wa miezi makumi ine na miwili.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ