Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 4:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Yesu akamujibu: “Imeandikwa hivi katika Maandiko Matakatifu: ‘Mutu hawezi kuishi kwa mukate tu, lakini kwa njia ya kushika kila neno Mungu analosema.’ ”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 4:4
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Waisraeli walipoona kitu kile wakashangaa, wakaulizana: “Nini hii?” Hawakujua kilikuwa kitu gani. Basi, Musa akawaambia: “Huu ni mukate ambao Yawe amewapa mukule.


Waisraeli walikula mana kwa muda wa miaka makumi ine, mpaka walipofika katika inchi iliyofaa kwa kuishi, ni kusema mpaka walipovuka mupaka wa Kanana.


Tena Musa akasema: “Magaribi, Yawe atawapa nyama mupate kula na asubui atawapa mikate mupate kula na kushiba. Maana yeye ameyasikia manunguniko muliyomunungunikia. Sisi ni nani hata mutunungunikie? Musitunungunikie sisi lakini mumunungunikie Yawe.”


Mutafanya sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kama vile nilivyowaagiza. Mutakula mikate isiyotiwa chachu kwa siku saba wakati uliopangwa katika mwezi wa Abibu, kwa sababu katika mwezi ule mulitoka Misri. Mutu yeyote asikuje mbele yangu mikono mitupu.


Kitu kinachoingia ndani ya kinywa cha mutu hakiwezi kumuchafua. Lakini ni kile kinachotoka ndani ya kinywa chake ndicho kinachomuchafua.”


Lakini Yesu akamwambia: “Toka wewe, Shetani! Kwa maana imeandikwa: ‘Umwabudu Bwana Mungu wako na umutumikie yeye peke yake.’ ”


Yesu akamujibu: “Imeandikwa hivi vilevile: ‘Usimujaribu Bwana Mungu wako.’ ”


Yesu akaongeza kusema: “Ni kile kinachotoka ndani ya mutu ndicho kinachomuchafua.


Lakini Yesu akamujibu: “Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Usimujaribu Bwana Mungu wako.’ ”


Yesu akamujibu: “Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Mutu hawezi kuishi kwa mukate tu.’ ”


Lakini Yesu akamujibu: “Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Umwabudu Bwana Mungu wako na umutumikie yeye peke yake.’ ”


“Wakati Musaidizi nitakayewatumia toka kwa Baba atakapokuja, atanishuhudia mimi. Yeye ni Roho wa ukweli, naye anakuja toka kwa Baba.


Roho ndiye anayeleta uzima; mwili hauwezi kufaa kitu. Maneno haya niliyosema nanyi, ndiyo Roho na uzima.


Na yote yaliyoandikwa zamani katika Maandiko Matakatifu yameandikwa kwa ajili ya kutufundisha sisi, kusudi tuendelee kuchunga tumaini kwa njia ya kuvumilia na kufarijiwa sawa tunavyofundishwa katika Maandiko Matakatifu.


Mupokee wokovu kama vile kofia ya chuma ya kuwalinda, na Neno la Mungu kama upanga munaopewa na Roho.


Aliwazarau akawaacha muone njaa na kisha akawapa mana mukule, chakula ambacho hamukukijua, wala babu zenu hawajapata kukijua. Alifanya hivyo kusudi apate kuwafundisha kwamba mwanadamu haishi kwa mukate tu, lakini kwa kila neno Yawe analosema.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ