“Inchi ya Zebuluni na ya Nafutali, kufuata barabara inayokwenda kwenye ziwa, ngambo ya magaribi ya Yordani, katika jimbo la Galilaya, inchi ya watu wa mataifa mengine.
Siku ya Sabato ilipotimia, akaanza kufundisha katika nyumba ya kuabudia. Watu wengi waliomusikiliza, wakashangaa sana na kuulizana: “Huyu amepata maneno haya yote kutoka wapi? Ni hekima ya namna gani aliyopata? Ni kwa uwezo wa namna gani anafanya miujiza kama hii?
Kisha Yesu akaondoka kule katika jimbo lililokuwa karibu na Tiro, akapita Sidona na katikati ya inchi ya Miji Kumi, hata akafika kwenye ziwa la Galilaya.
Yesu akashuka toka kilima pamoja na wanafunzi wake, na kusimama kwenye uwanja. Pale kulikuwa wanafunzi wake pamoja na kundi kubwa sana la watu waliotoka Yerusalema, katika Yudea yote na pande za miji Tiro na Sidona pembeni ya bahari.