Basi, Elisha akamwacha Elia, akarudilia ngombe wake, akawachinja ngombe hao na kuwapika akitumia miti ya nira kama kuni, akawapa watu, wakakula. Kisha akaondoka, akamufuata Elia na kuwa mutumishi wake.
“Yeye anayemupenda baba yake au mama yake kuliko mimi, hastahili kuwa wangu, na yeyote anayemupenda mwana wake au binti yake kuliko mimi hastahili kuwa wangu vilevile.
Yesu alipoendelea mbele kidogo, akawaona wandugu wengine wawili, Yakobo na Yoane, waliokuwa wana wa Zebedayo. Walikuwa ndani ya chombo pamoja na baba yao Zebedayo, wakitengeneza nyavu zao. Yesu akawaita.