Matayo 4:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
15 “Inchi ya Zebuluni na ya Nafutali, kufuata barabara inayokwenda kwenye ziwa, ngambo ya magaribi ya Yordani, katika jimbo la Galilaya, inchi ya watu wa mataifa mengine.
mufalme Solomono alimupa Hiramu mufalme wa Tiro miji makumi mbili katika jimbo la Galilaya kwa sababu yule Hiramu alikuwa amemupelekea Solomono mbao za mierezi na miberoshi, na zahabu vilevile, kadiri alivyohitaji kwa majengo.
Wakati wa utawala wa Peka mufalme wa Israeli, Tigilati-Pileseri, mufalme wa Asuria, aliteka miji ya Iyoni, Abeli-Beti-Maka, Yanoa, Kadesi na Hazori, pamoja na inchi za Gileadi, Galilaya na Nafutali na kuwahamisha wakaaji wake kwenda Asuria.
Kisha akawaelezea maneno yaliyoandikwa juu yake katika Maandiko Matakatifu yote, akianza toka vitabu vya Musa na kuendelea katika vitabu vya manabii wote.
Basi, kwa ajili hiyo wakaitenga miji ya Kedesi katika Galilaya kwenye milima ya Nafutali, Sekemu katika milima ya Efuraimu na Kiriati-Arba, ni kusema Hebroni, katika inchi ya milima ya Yuda.
Katika eneo la kabila la Nafutali walipewa Kedesi, muji wa kukimbilia usalama unaokuwa kule Galilaya pamoja na mbuga zake za malisho, Hamoti-Dori pamoja na mbuga zake za malisho na Kartani pamoja na mbuga zake za malisho. Kwa jumla, miji mitatu.