Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Matayo 4:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Lakini Yesu akamwambia: “Toka wewe, Shetani! Kwa maana imeandikwa: ‘Umwabudu Bwana Mungu wako na umutumikie yeye peke yake.’ ”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Matayo 4:10
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Shetani akaenda kinyume cha Waisraeli, akamushawishi Daudi kuwahesabu watu.


Yawe akamwambia Shetani: “Basi, unaweza kufanya vile unavyotaka juu ya mali yake. Lakini tu yeye mwenyewe usimuguse.” Basi, Shetani akaondoka mbele ya Yawe.


Basi, ikatukia siku moja wamalaika wa Mungu walikwenda kukutana mbele ya Yawe. Shetani akakuja kuwa pamoja nao.


Ikatokea tena siku ingine, wamalaika wa Mungu walikwenda kukutana mbele ya Yawe. Shetani akakuja kuwa pamoja nao.


Umuweke mwamuzi mubaya juu ya adui yangu; na anayemushitaki amupeleke mbele ya baraza.


Mutanitumikia mimi Yawe, Mungu wenu, nami nitawabariki kwa chakula na maji na kuondoa magonjwa kati yenu.


Mutazihesabu sanamu zenu za miungu zilizopakwa feza na zahabu kuwa uchafu. Mutazitupilia mbali kama takataka, mukisema: Mupotelee mbali!


Lakini Yesu akageuka na kumwambia: “Ondoka hapa karibu nami, wewe Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu, kwa maana mawazo yako si ya Mungu, lakini ni ya kimutu.”


Akabaki katika jangwa kwa muda wa siku makumi ine, na kule Shetani akamujaribu. Alikaa kule katikati ya nyama wa pori, nao wamalaika walimushugulikia.


Naye Yesu akamwambia: “Nilimwona Shetani akianguka kama umeme toka mbinguni.


Basi ikiwa Shetani akijigombanisha mwenyewe, ufalme wake hautadumu. Ninasema hivi, kwa maana ninyi munasema kama ninafukuza pepo kwa uwezo wa Belzebuli.


Sasa, mwanamuke huyu anayekuwa wa uzao wa Abrahamu, ambaye alifungwa na Shetani kwa muda wa miaka kumi na minane, haikumupasa afunguliwe katika kifungo hiki ingawa ni siku ya Sabato?”


Basi Shetani akamwingia Yuda, yule anayeitwa Iskariota, aliyekuwa mumoja wa wanafunzi kumi na wawili.


“Simoni, Simoni! Sikiliza: Shetani ameachiliwa wakati wa kuwajaribu na kuwatenga kabisa.


Lakini Yesu akamujibu: “Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Umwabudu Bwana Mungu wako na umutumikie yeye peke yake.’ ”


Yuda alipokwisha kukamata kile kipande cha mukate, Shetani akamwingilia. Basi Yesu akamwambia: “Unayotaka kufanya, uyafanye upesi!”


kusudi ufungue macho yao, ukiwaongoza watoke katika giza na kuwaingiza katika mwangaza. Watatoka chini ya uwezo wa Shetani na kumugeukia Mungu, kusudi kwa njia ya kuniamini wapate kusamehewa zambi zao na kupewa urizi pamoja na watu wake watakatifu.’


Basi Petro akamwuliza: “Anania, namna gani Shetani amekuingia hata akakusemesha uongo mbele ya Roho Mutakatifu na kuficha sehemu ya feza ulizopata ulipouzisha lile shamba?


Basi munapaswa kumutoa mutu yule kwa Shetani, kusudi mwili wake uharibiwe, nayo roho yake iweze kuokolewa Siku ile Bwana Yesu atakaporudi.


Musinyimane, isipokuwa tu mumepatana na kwa muda tu kusudi mupate wakati wa kujitoa kwa kufunga na kuomba. Kisha munaweza kurudiliana tena kusudi Shetani asiwajaribu katika uzaifu wenu.


Na jambo hilo si la kushangaza kwa maana Shetani mwenyewe anajisingizia kuwa malaika wa mwangaza.


Lakini, kusudi nisijivune kupita kipimo kwa ajili ya kupokea ufunuo wa ajabu, nilitiwa katika mwili wangu kitu kinachoniumiza kama mwiba. Kitu kile ni kama mujumbe wa Shetani kwa kunipiga na kunizuiza nisijivune kupita kipimo.


kusudi Shetani asipate njia ya kutushinda, maana tunajua nia zake.


Mumwogope Yawe, Mungu wenu, mumutumikie, muambatane naye na kuapa kwa jina lake.


Basi mumutii Mungu. Mupingane na Shetani, naye atawakimbia.


“Sasa, basi, mumutii Yawe na kumutumikia kwa moyo wa haki na uaminifu. Muache kabisa miungu ile ambayo wazee wenu waliiabudu ngambo ya muto Furati na katika inchi ya Misri. Mumutumikie Yawe.


Mupingane naye, mukisimama imara katika imani, mukijua kwamba fasi zote katika dunia, wandugu zenu wanapata mateso kama hayo.


Samweli akawaambia Waisraeli: “Kama munamurudilia Yawe kwa moyo wenu wote, basi mutupilie mbali miungu ya kigeni na sanamu za Astaroti. Muelekeze mioyo yenu kwa Yawe, na kumutumikia yeye peke yake; naye atawaokoa kutoka katika mikono ya Wafilistini.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ