Matayo 3:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
12 Yeye anashika lungo katika mikono yake kwa kupepeta ngano. Atakusanya ngano na kuitia katika gala yake, lakini atateketeza maganda katika moto usiozimika.”
Wenye nguvu watakuwa kama majani yenye kukauka, matendo yao yatakuwa kama cheche za moto. Watateketea pamoja na matendo yao, wala hakutakuwa mutu wa kuwaokoa.
Mataifa yananguruma kama ngurumo ya maji mengi, lakini Mungu atayakaripia, nayo yatakimbilia mbali. Yatafukuzwa kama maganda juu ya mulima mbele ya upepo; kama mavumbi yanayonyanyuliwa na upepo mukali.
Mulimaji anapopepeta ngano yake, haendelei kuipepeta mpaka kuvunja punje zake. Anajua jinsi ya kuipepeta kwa gurudumu la gari, bila kuharibu punje za ngano.
Mutaipepeta milima hiyo, nao upepo utaipeperushia mbali, zoruba itaitawanya huko na huko. Nanyi mutafurahi kwa sababu yangu Yawe; mutaona utukufu kwa sababu yangu Mungu Mutakatifu wa Israeli.
Kwa hiyo, kama vile moto unavyoteketeza nyasi, kama vile majani yanavyotoweka ndani ya moto, ndivyo mizizi yao itakavyooza, na maua yao yatakavyopeperushwa juu kama mavumbi. Maana wameacha sheria ya Yawe wa majeshi, wamezarau neno la yule Mutakatifu wa Israeli.
Kisha watakwenda kuziona maiti za wale walioniasi. Wadudu watakaowakula hawatakufa, na moto utakaowachoma hautazimika hata kidogo. Watakuwa chukizo kwa watu wote.
Nimepepeta watu wangu kwa kuwasambaza sawa maganda, toka katika kila muji wa inchi yao. Nimewaangamiza kwa kuwaua watoto wao, lakini hawakuacha mwenendo wao.
Lakini musiponisikiliza na mukiacha kuihesabu siku ya Sabato kama siku takatifu, musipoacha kubeba mizigo na kuingia nayo kupitia milango ya Yerusalema siku ya Sabato, basi nitawakisha moto katika milango yake, nao utateketeza nyumba zote nzuri za Yerusalema, wala hautazimika. –Ni ujumbe wa Yawe.
Wakati huo, wataambiwa hivi watu hawa pamoja na muji Yerusalema: Upepo wenye kuunguza kutoka vilele vya milima katika jangwa utawavumia watu wangu. Huo si upepo mudogo wa kupepeta ngano,
Nitawapeleka wapepetaji katika inchi ya Babeli, nao watamupepeta; watamaliza kila kitu katika inchi yake watakapofika kuishambulia toka kila upande wakati wa maangamizi yake.
Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitaimwanga hasira yangu juu ya pahali hapa, juu ya wanadamu na nyama, miti katika mashamba na juu ya mazao ya inchi. Nayo nafasi hii itawaka moto wala hautaweza kuzimishwa.
Basi, watatoweka kama ukungu wa asubui, kama umande unaotoweka upesi; kama makapi yanayopeperushwa kwenye nafasi ya kupepetea, kama moshi unaotoka katika munara wa kutoshea moshi inje.
Muviache vyote viwili vikomae pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati ule nitawaambia wavunaji: muongoe kwanza nyasi, nanyi muzilundike kwa mafungu mafungu kwa kuzichoma, na kisha mukusanye ngano na kuweka mavuno ndani ya gala yangu.’ ”
Mwana wa Mutu atawatuma wamalaika wake, nao watakusanya toka katika Ufalme wake watu wote wanaowaangusha wengine katika zambi pamoja na wote wanaofanya maovu.
Basi Yoane akawaambia wote: “Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini yule atakayekuja nyuma yangu ni mwenye uwezo kunipita; nami sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mutakatifu na kwa moto.